Ruka hadi kwenye maudhui makuu

ROONEY SASA KUTUA ARSENAL

MSHAMBULIAJI Wayne Rooney (Pichani)  ataamua kwenda Arsenal iwapo tu ndoto zake za kufanya kazi na Jose Mourinho Chelsea litabuma.

Manchester United imekataa kumuuza Rooney kwa wapinzani wake wakuu kwenye mbio za ubingwa, lakini mshambuliaji huyo bado anataka kuondoka Old Trafford.
Pamoja na kwamba Chelsea ni chaguo la kwanza, mshambuliaji huyo wa England atakwenda Arsenal iwapo David Moyes na bodi ya United itakaata ofa nyingine ya Mourinho.
Departing? Wayne Rooney is a target for both Arsenal and Chelsea
Anaondoka? Wayne Rooney anatakiwa na Arsenal na Chelsea
Arsenal ilitia mkono kwa Rooney, ambaye atatimiza miaka 28 mwaka huu, wakati alipowekwa benchi katika mazingira ya kutatanisha kwenye mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa nyumbani dhidi ya Real Madrid, Machi. 
Arsenal imesema inaweza kulipa mshahara wa Rooney, anayelipwa Pauni 240,000 kwa wiki na amebakiza miaka miwili katika Mkataba wake wa sasa. 
Chelsea wanabaki kileleni katika ushindani wa ofa kubwa, wakiwa wametoa Pauni Milioni 23, jumlisha Pauni 2.5 zitakazoongezwa kwa vipengele.
Baada ya kuumia nyama, Rooney alirejea kufanya mazoezi mepesi katika Uwanja wa United, Carrington na ni matumaini klabu hizo mbili zitafikia makubaliano. Mkewe, Coleen anafurahia maisha ya London na mtoto wao kwa manufaa ya kazi yake.
Jose Mourinho
Arsene Wenger
Ushindani: Jose Mourinho na Arsene Wenger wote wanapenda kumsaini Rooney kutoka United
Ubora wa nyota huyo ndio unaomfanya Mourinho ajaribu kumhamishia Rooney Chelsea, lakini pia anamheshimu Arsene Wenger.
Mshambuliaji huyo wa England, ambaye anaweza kuwa fiti kucheza wiki mbili zijazo, ameambiwa kocha wa Arsenal, Wenger atajenga timu yake kwa kumhusisha yeye.
Hiyo inafuatia Rooney kusukumwa nje ya kikosi cha kwanza na Sir Alex Ferguson na hadhi yake kushuka chini ya kocha mpya, David Moyes.
Under pressure? David Moyes could be on the verge of losing one of his best players
David Moyes yuko kwenye hatari ya kupoteza moja ya nyota wake
Rooney alifanya mawasiliano ya simu Moyes na Makamu Mwenyekiti, Ed Woodward baada ya kuibuka taarifa kwamba mshambuliaji huyo amekasirika kutokana na namna anavyochukuliwa katika klabu hiyo.
Chelsea inajiandaa kuongeza ofa yake kwa ajili ya Rooney, lakini haitakuwa tayari kuzidisha Pauni Milioni 30. Ikiwa United itakataa kumuuza Chelsea- Arsenal watakuwa kwenye nafasi nzuri ya kumpata.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC