Ruka hadi kwenye maudhui makuu

RAGE AFUTA NDOTO YA SIMBA KUMILIKI UWANJA WAKE, KAULI YAKE YAZUA UTATA CCM

Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage (Pichani) ameifuta ndoto ya klabu hiyo kuwa na uwanja wake, baada ya kusema haiwezekani uongozi wake kujenga uwanja katika miaka miwili wakati Serikali imejenga Uwanja wa Taifa kwa miaka 50.
Rage alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki kwenye mkutano mkuu wa klabu hiyo uliofanyika Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay huku ukitawaliwa na vurugu zilizosababisha ajenda za muhimu za mkutano kushindwa kujadiliwa kwa kina.
‘’ Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi CCM imewachukua miaka 50 kujenga uwanja wa kisasa ule wa Taifa, sasa mimi Rage na Kamati yangu tutajenga uwanja wa kisasa kwa miaka miwili uwezo huo tunatolea wapi? “alihoji “Vitu vingine vinahitaji kufikiria kwa kawaida tu jamani. Tunaomba muwe wavumilivu tunaenda polepole, lakini kwa uhakika tumeshalipia eneo la ujenzi tunasubiri hati yetu.
Kauli hiyo ilizua majadiliano kutoka kwa wajumbe, lakini Rage aliendelea kusema  ‘’nipo kwenye agenda ya saba nyie pigeni kelele tu mimi naendelea (huku akicheka).
Hapa kuna watu wanataka kwenda kuangalia mpira, tena mtaingia bure na  vitambulisho vyenu, vya mkutano, Simba oyeeee’’.
Licha ya Rage kutoa kauli hiyo, mwenyekiti huyo amekuwa akitoa kauli tofauti tangu alipoingia madarakani juu ya ujenzi wa uwanja huo ambao umebaki kuwa ni ndoto.
Baadhi ya kauli zake ambazo amewahi kuzitoa ni hizi, Desemba 17/2010, alisema mradi wa kujenga uwanja huko Bunju kwa ajili ya timu yao unaendelea vizuri, lakini  mwekezaji wao kutoka Uturuki ambaye alitarajia kuja hivi karibuni atawasili mwakani mara baada ya kupita Sikukuu za Krismas na Mwaka Mpya.
 “Kwa sasa tumebuni mradi ambao utasaidia kupata fedha kama sh 100 milioni ambazo zinatakiwa kulipia uwanja wetu.
 Mradi huo ni uuzwaji wa jezi ambazo zitauzwa kati ya sh10,000 na 15,000 kwa wanachama wa Simba kwa ajili ya kuchangia gharama za kulipia kitalu hicho.
Novemba 29/2010, Rage alitangaza mipango ya kujenga uwanja wa kisasa wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 30,000, eneo la Bunju na ujenzi utasimamiwa na Kampuni ya Uturuki GIDS, na akajikamba ni mabingwa wa ujenzi wa viwanja.
“Uwanja utazungukwa na maduka ya kisasa (Mall) na aliunda timu akiwemo aliyekuwa Makamu Mwenyekiti aliyebwaga manyanga Geofrey Nyange ‘Kaburu’, Francis Waya, Katibu Mkuu wao Evodius Mtawala.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC