Ruka hadi kwenye maudhui makuu

POULSEN AENDELEA KUMBEBA JUMA KASEJA

Kocha wa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Kim Poulsen amesisitiza kuwa kipa na nahodha wa timu hiyo, Juma Kaseja (Pichani) bado yuko katika kiwango cha juu na ndiye chaguo lake la kwanza licha ya kuachwa na klabu yake ya Simba katika kikosi chao cha msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.


Poulsen aliyasema hayo jana jijini Mwanza wakati Stars ikikaribia kwenda Uganda kujiandaa kwa mechi yao ya keshokutwa dhidi ya wenyeji (The Cranes) kuwania kufuzu kwa fainali zijazo za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ligi za ndani (CHAN).

Poulsen alisema kuwa kiwango cha Kaseja kimekuwa kikiongezeka kadri siku zinavyokwenda na hiyo inatokana na uzoefu alio nao katika umri wake wa sasa wa miaka 29.

Kocha huyo aliongeza kuwa kwa nafasi ya kipa, umri wa Kaseja ndiyo mzuri zaidi kwani mchezaji wa kiwango cha juu kama yeye anakuwa tayari ameshapata uzoefu wa kutosha kutokana na mechi nyingi alizocheza katika ligi mashindano ya kimataifa.

"Angalia kiwango chake... bado ni cha juu na siku hadi siku anazidi kuimarika. Angalia alivyofanya vizuri tulipocheza dhidi ya timu kubwa kama Cameroon. Kwa ujumla timu nzima inajengeka na yeye uzoefu wake ni muhimu zaidi," alisema kocha huyo raia wa Denmark.

Hivi karibuni, uongozi wa Simba ulitangaza kumuacha Kaseja kwa kutompa mkataba mwingine wa kuidakia timu hiyo aliyotumikia kwa takriban muongo mmoja.

Katika hatua nyingine, Poulsen alikiri kwamba kutoroka kambini kwa kiungo Mwinyi Kazimoto wa Simba kumemuharibia mipango yake kwani sasa watalazimika kuziba nafasi yake kwa usahihi na pia wanapaswa kupangua safu ya ulinzi baada ya kuondoka kwa beki Shomari Kapombe anayetarajiwa kufanyiwa majaribio ya kucheza soka la kulipwa nchini Uholanzi.

"Siwezi kusema tutatumia mfumo gani (dhidi ya Uganda) kwa sababu tutakuwa tunatoa siri kwa wapinzani wetu. Ila naamini tutafanya vizuri katika mechi hii ya ugenini," aliongeza, huku akiliacha suala la kutoroka Kazimoto kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Stars ilifungwa goli 1-0 katika mechi yao ya kwanza dhidi ya Uganda iliyochezwa Julai 13 kwenye Uwanja wa Taifa na hivyo watalazimika kujibu mapigo kwa kushinda keshokutwa kwa walau 2-0 ili wasonge mbele katika michuano ambayo fainali zake zitafanyika mwakani nchini Afrika Kusini.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC