Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NEEMA KUBWA YAMWANGUKIA KASEJA

 
Kipa chaguo la kwanza wa timu ya taifa ya soka ya Tanzania (Taifa Stars), Juma Kaseja (Pichani) , ambaye hivi sasa yuko huru baada ya kumaliza mkataba wake wa kuidakia Simba amepata ofa nono ya dola za Marekani 30,000 (Sh. milioni 50) kutoka kwa klabu ya FC Lupopo inayoshiriki Ligi Kuu ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ili aanze kuitumikia msimu ujao, imefahamika.


Kaseja amepata ‘ulaji’ huo kufuatia uongozi wa FC Lupopo kuachana na kipa wa Mtibwa Sugar, Hussein Shariff 'Cassilas' ambaye hawakukubaliana dau la uhamisho na klabu yake ya Mtibwa ya Manungu, Turiani mkoani Morogoro.

Inadaiwa kuwa Lupopo walikuwa tayari kumsajili Shariff kwa dola za Marekani 20,000, lakini baadaye Mtibwa Sugar walitaka kiasi kama hicho ili wavunje mkataba naye jambo ambalo klabu hiyo ya Kongo haikuwa tayari kwani maelezo ya awali waliyokuwa nayo ni kwamba kipa huyo alikuwa hana timu.

Habari zilizopatikana jana jijini Dar es Salaam zinasema kuwa Kaseja ambaye alimaliza mkataba wa kuichezea Simba tangu Juni 30 mwaka huu atalipwa mshahara wa kila mwezi wa dola za Marekani 2,000 (Sh. milioni 3.2), kiasi ambacho inadaiwa ni kikubwa kulinganisha na mshahara aliokuwa akilipwa na klabu yake ya zamani ya ‘Wekundu wa Msimbazi’.

Chanzo hicho kilifichua zaidi kwamba uongozi wa Lupopo tayari umeshafanya mazungumzo ya awali na Kaseja na hivyo kipa huyo nyota wa Stars anasubiriwa afike ili amalizane nao na kusaini mkataba.

"Hata hivyo, watu wa Lupopo wamekuwa wakimbembeleza kipa huyo ili wampe mkataba wa miaka miwili… mwenyewe Kaseja anataka asaini mkataba wa kuichezea kwa mwaka mmoja tu, ila dalili zinaonyesha watakubaliana kwavile hii ni ofa nzuri kwake (Kaseja) kwa wakati huu," kilisema chanzo hicho.

Akizungumza na mtandao huu kutokea Kampala jana mchana, Kaseja alikiri kufanya mazungumzo na timu moja ya nje ya nchi na nyingine kadhaa za hapa nchini, lakini hakutaka kuzitaja timu hizo kwa maelezo kuwa bado hajahitimisha majadiliano.

Kaseja alisema vilevile kuwa baadhi ya timu zimeshindwa kufanya naye mazungumzo rasmi kwa kuhofia gharama za kumsajili, ingawa wengi wao wameonyesha kuwa kiufundi wanamhitaji sana.

"Hapa bongo zipo timu zinanisubiri nirudi ili tufanye mazungumzo na klabu moja ya nje ya nchi pia inanihitaji. Sema timu nyingi zinaniogopa kwavile wanahisi kwamba siwezi kuzikubalia au labda nitataka pesa nyingi kutokana na uzoefu wangu langoni," alisema Kaseja.

Ingawa Kaseja hakutaja timu zinazomhitaji, lakini inafahamika wazi kuwa mojawapo ni klabu ya Mbeya City ya Mbeya iliyopanda daraja na kucheza Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu ujao. Kocha wa klabu hiyo, Juma Mwambusi, amekuwa akisema kuwa wanamuhitaji kipa huyo kwavile bado yuko katika kiwango cha juu na uzoefu wake utawasaidia sana kikosini.

Licha ya kuidakia Simba kwa takriban muongo mmoja, Kaseja pia aliwahi kuzichezea Moro United iliyokuwa Morogoro na Yanga aliyoitumikia kwa msimu mmoja.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC