Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAN UNITED YANUSURIKA KICHAPO



Bao la dakika za lala salama kutoka kwa Wilfried Zaha liliokoa Manchester United kutoka kwa kichapo cha aibu cha tatu katika ziara yao ya kipindi cha kabla ya msimu bara Asia mnamo Ijumaa, na kutoka sare 2-2 na Cerezo Osaka timu aliyochezea Shinji Kagawa katika Ligi-J.

Kagawa, aliyehamia Old Trafford kutoka Borussia Dortmund mwaka mmoja uliopita, pia alisisimua mashabiki 44,856 waliofurika uwanja wa Nagai kwa kufungia United bao lake la kwanza baao ya kupoteza penalti kwa kupiga mkwaju moja kwa moja hadi mikononi mwa kipa wa Osaka Kim Jin-Hyeon.
Red Devils sasa wameshinda mechi mbili na kushindwa mbili Asia baada ya kupoteza 1-0 mikononi mwa timu ya All Stars wa Ligi ya Thailand wiki mbili zilizopita mjini Bangkok, wakawalemea All Stars wa Ligi A mjini Sydney na tena wakawainamia Yokohama Marinos wa Ligi J Jumane iliyopita.
Straika wa Cerezo Kenyu Sugimoto alifungua ukurasa wa mabao kunako dakika ya 34 kwa kuwachenga walinzi wawili na kutoa kombora kwa guu la kushoto ambalo lilimpita Lindegaard baada ya kunasa pasi iliyokuwa imetolewa na Chris Smalling wa United.
United nusura wasawazishe dakika ya 40 pale Kagawa alipotoa kombora la juu baada ya straika Mholanzi Robin van Persie kumwandalia mpira maridadi alioupata kutoka kwa mpira uliodunda kutoka kwa kombora la Danny Welback mlingoti wa kushoto.
Kagawa alipoteza penalti dakika ya 53 pale Ashley Young alipochezewa visivyo eneo la hatari na difenda wa Cerezo Tatsuya Yamashita.
Lakini Mjapani huyo wa umri wa miaka 24 alijirejeshea hadhi yake kwa kufunga dakika mbili baadaye, kwa kutuma mpira wavuni kupitia katikati ya miguu ya Kim baada ya kupata mpira ulioandaliwa na Ryan Giggs.
Dakika chache baadaye, Kagawa alitolewa uwanjani huku akishangiliwa na mashabiki wake wa zamani, na muda si muda Cerezo wakawashangaza mabingwa hao wa Uingereza kwa bao la pili kupitia mshambuliaji wa umri wa miaka 18 Takumi Minamino dakika ya 63.
Kombora la Minamino kutoka upande wa kushoto nje ya eneo la hatari lilielekea juu ndani ya wavu. Lakini Zaha aliwaliwaza wageni na kuwaokoa kutoka kwa aibu kwa kufunga bao la kusawazisha dakika moja kabla ya mechi kumalizika baada ya kupata mpira ulioandaliwa na Jesse Lingard.
Katika mechi yao ya mwisho ziara yao ya Asia, mabingwa hao wa Uingereza watacheza dhidi Kitchee FC mjini Hong Kong mnamo Jumatatu na kuhitimisha kampeni yao ya kabla ya msimu kwa mechi ya kirafiki dhidi ya AIK Fotboll ya Sweden mjini Stockholm Agosti 6.
United chini ya David Moyers – aliyeteuliwa mrithi wa kocha wa muda mrefu Alex Ferguson mwishoni mwa msimu uliopita – ataanza kampeni yake ya kutetea taji dhidi ya Swansea City ugenini Agosti 17.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC