Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KIMEELEWEKA, HATIMAYE FABREGAS KUNUKIA MAN UNITED

Uncertain future: Cesc Fabregas could leave Barcelona for Manchester UnitedKIUNGO Cesc Fabregas amewaambia rafiki zake England kwamba anataka kuondoka Barcelona kuhamia Manchester United.

Kiungo huyo wa Hispania kwa sasa anagombewa na United na Barcelona, na mabingwa hao wa Ligi Kuu y England wamekwishatoa ofa ya Pauni Milioni 30.
Kocha wa United, David Moyes aliwaambia Waandishi wa Habari nchini Japan jana kwamba mpango wa klabu hizo kufanya biashara ya nyota huyo wa zamani wa Arsenal unaendelea na ofa nyingine itatolewa.
Lakini habari kwamba Fabregas amewaambia rafiki zake England kwamba anataka kuondoka Nou Camp hatimaye zinaweza kuwapa faraja United.
Inafahamika Fabregas anavutiwa na ahadi ya kuwa na namba ya kudumu kwenye kikosi cha kwanza United na yuko tayari kuungana na mchezaji mwenzake wa zamani wa Arsenal, mshambuliaji wa United, Robin van Persie.
Fabregas pia anaamini anaweza kutwaa taji la England na United kuunganisha na lile moja aliloshinda Hispania la La Liga msimu uliopita. 
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ameshinda taji la FA na Ngao ya Jamii pekee katika kipindi chake cha kuichezea Arsenal.
Barcelona wameendelea kutia kauzibe wakiiambia United kwamba, kiungo wao hawamuuzi."Vidic, Nani nad Antonio Valencia wote wanacheza nao. Wayne Rooney pia anakimbia na katika kiwango ambacho tunafikiri atakuwa fiti. Atapiga hatua wiki hii,".
Lure: The prospect of linking up with Robin van Persie again is tempting Fabregas
Muungano wawezakana: Uwezekano wa Robin van Persie kuungana na Fabregas tena wawezekana
New-look United: David Moyes and Steve Round are now in charge at Old Trafford
Muonekano mpya United: David Moyes na Steve Round sasa ni makocha Old Trafford
Fond memories: Van Persie and Fabregas combined with success at Arsenal
Watarudisha enzi: Van Persie na Fabregas walifanya kazi pamoja kwa mafanikio Arsenal
Talented squad: Fabregas may also be tempted by the chance to win trophies in English football
Kikosi cha vipaji: Fabregas pia anaweza kuvutiwa na hamu ya kushinda katika soka ya England

Iwapo Fabregas ataamua kuomba kuondoka, mambo yanaweza kubadilika.
United inatarajiwa kucheza mechi yake ya nne katika ziara yake ya kujiandaa na msimu, leo ikimenyana na Cerezo Osaka saa 5:00 asubuhi za Uingereza.
Van Persie anatarajiwa kucheza sehemu kidogo baada ya kupata ahueni ya maumivu yake, wakati Moyes pia amesema kwamba Nahodha wake, Nemanja Vidic — ambaye pia amekuwa majeruhi ameanza kucheza soka ya ushindani nyumbani England.
Moyes alisema: "Kunakuwa kuna mechi za mazoezi siku nyingine Carrington. 
New kit: There have been many changes around United since the end of the season
Jezi mpya: Kuna mabadiliko mengi United tangu mwishoni mwa msimu
Bullet train: The United squad have been travelling through Japan in style
Treni ya umeme: Kikosi cha United kimekuwa kikisafiri kwa staili ya aina yake Japan 
Talented: Fabregas is among the finest midfielders in the world

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC