Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA BADO HAIJAPATA BEKI WA KATI-KIBADEN

Kocha wa klabu ya Simba, Abdallah Kibadeni (Pichani), amesema kikosi chake kipo tayari kwa ligi kuu ya Bara lakini bado anahitaji beki wa kati mwenye uwezo mkubwa.


Akizungumza  kwa njia ya simu kutoka kambini Kigamboni jiji la Dar es Salaam, Kibadeni alisema amepata kikosi chake cha kwanza lakini anataka kuongeza nguvu kwenye safu ya ulinzi ya timu hiyo.

"Tumefanya mazoezi kwa muda mrefu sasa na tayari nimewafahamu wachezaji wangu na uwezo wao," alisema Kibadeni ambaye ni kocha bora wa mwaka jana kwa kuiwezesha Kagera Sugar kushika nafasi ya nne licha ya udogo wa timu.

"Kwangu timu imekamilika na vitu vilivyobakia ni kidogo sana... naangalia sana safu yangu ya ulinzi."

Alisema ameshatoa maombi kwa uongozi wa timu hiyo ili kutafutiwa beki wa kati na kwamba viongozi hao wapo kwenye mazungumzo na baadhi ya wachezaji wa nje ya nchi kwa ajili ya kuona uwezekano wa kuwasajili.

Mmoja wa mabeki wa kati ambao Simba kwa sasa ipo kwenye mazungumzo nao ni mchezaji wake wa zamani, Joseph Owino wa URA ya Uganda.

Owino aliwahi kuichezea kwa mafanikio Simba miaka miwili iliyopita kabla ya kuachwa na kwenda Azam msimu mmoja, na kurudi Uganda kujiunga na URA.

Kibadeni alisema anataka Simba isajili beki mwenye uwezo na uzoefu ili kuisaidia timu kwenye ligi kuu inayatorajiwa kuanza Agosti 24.

Alipoulizwa juu ya Owino, Kibadeni alisema uongozi wa klabu hiyo unamfuatilia mchezaji huyo na kusema endapo atasajiliwa kwenye timu hiyo atakuwa msaada mkubwa katika harakati za kutaka kutwaa ubingwa msimu huu.

Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu hiyo, Zacharia Hanspope alikaririwa na vyombo vya habari akisema wanafanya mazungumzo na Owino kwa lengo la kumsajili baada ya kuwasiliana na Kibadeni.

Wakati Simba wakitafuta beki wa kati, kikosi hicho pia kipo hatarini kumpoteza beki wake kiraka, Shomari Kapombe ambaye amekwenda kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa nchini Uholanzi.

Endapo Kapombe atafanikiwa na kupata timu nchini humo, Simba itawalazimu kutafuta mbadala wake.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC