Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KASEJA ATOBOA SIRI YA KIPIGO CHA JANA

NAHODHA wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Juma Kaseja (Pichani akiangalia mpira ukitinga kimiani)  amewataka mashabiki wa soka nchini kubadilisha mitazamo yao kwamba wachezaji chupikizi ndiyo wanaofaa kuliko wakongwe.Akizungumza jana mjini hapa, Kaseja alisema kwamba mashabiki wamekuwa wakitaka sana wachezaji chipukizi wapewe nafasi, lakini ukweli ni kwamba hawamudu kabisa.



“Tusaidieni kuwaelimisha mashabiki, wao wanataka sana wachezaji chipukizi, lakini nadhani mmeona leo, hawawezi. Wanahitaji kupewa muda wakomae taratibu. Hata sisi tulipokuwa chipukizi, tulikomazwa taratibu,”alisema Kaseja.
Ingawa Kaseja hakuweka wazi, lakini inaonekana alikuwa anawazungumzia wachezaji chipukizi walivyoigharimu Stars jana ikitolewa na Uganda katika michuano ya Ubingwa wa Mataifa ya Afrika (CHAN), inayohusisha wachezaji wanaocheza ligi za nchini mwao pekee, ikafungwa na Uganda mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole mjini hapa.
Kwa matokeo hayo, Tanzania inayofundishwa na kocha Mdenmark, Kim Poulsen imetolewa kwa jumla ya mabao 4-1, baada ya wiki mbili zilizopita kufungwa 1-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Beki chipukizi, David Luhende aliyeitwa Stars kwa mara ya kwanza safari hii, aliunawa mpira akiwa peke yake- baada ya kushindwa kuumilii vyema na kusababisha penalti, wakati huo timu hizo zikiwa zimefungana 1-1 na Brian Majwega akaifungia Uganda bao la pili.

Kiungo chipukizi, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ aliyepandishwa timu hiyo Mei mwaka jana, alijaribu kuwapiga chenga wachezaji wawili wa Uganda, wakati huo wachezaji karibu wote wa Tanzania wamepanda kufuata shambulizi la kona, akapokonywa mpira na likafanywa shambulizi la kushitukiza, Stars ikafungwa bao la tatu.
Wachezaji wengine chipukizi walioingizwa kipindi cha pili, Simon Msuva na Haroun Chanongo walishindwa kuisaidia timu kubadilisha matokeo japo kidogo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC