Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HUMUD SAFI SIMBA, KULAMBA MAMILIONI KUICHEZEA MSIMU UJAO

Kiungo mkabaji wa zamani Azam FC, Abdulhalim Humoud (Pichani) ameibukia Simba akisaka nafasi ya kusajiliwa kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

Humoud aliyemaliza mkataba wake na Azam FC Mei, mwaka huu na kwenda Afrika Kusini kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa na klabu ya Jomo Cosmos, yuko kambi ya Simba iliyopo, Kigamboni, Dar es Salaam.
Akizungumza jana, Makamu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang’are alithibitisha mchezaji huyo kuwepo kwenye kambi ya timu yake akisaka nafasi kwa ajili ya msimu ujao wa ligi,  Agosti 24.
Itang’are alisema kuwa Kocha Abdallah Kibadeni ndiye aliyemtaka mchezaji huyo anayedaiwa kufuzu na klabu ya Jomo Cosmos.
“Kocha ndiye ametaka aje kambini kufanya mazoezi na timu ili aweze kujiridhisha na kiwango chake kabla ya kusaini mkataba,” alisema na kuongeza.
“Kamati ya Usajili Simba, tunasubiri kauli ya mwisho kutoka benchi la ufundi na kufanya naye makubaliano ya kusaini mkataba.”
Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah Kibadeni alisema jana kuwa, yuko kwenye kambi ya Simba kwa siku tano sasa akifanya mazoezi na wachezaji wenzake.
“Maendeleo yake ni mazuri ingawa siwezi kusema lolote kwa sasa. Ni mchezaji ambaye namjua vizuri, siyo mgeni kwangu. Pia najua aliwahi kuichezea Simba kipindi cha nyuma kabla ya Azam FC.” alisema Kibadeni.
Humoud alipofuatwa na gazeti hili baada ya kumaliza mazoezi alisema: “Sitaki kuzungumza lolote kwa sasa, ni mapema.”
Humoud alijiunga na Simba akitokea Mtibwa Sugar na kutolewa kwa mkopo na klabu hiyo kwenda Azam FC.
Wakati huohuo, mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Hussein Javu amejiunga na mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga na jana asubuhi alifanya mazoezi.
Javu aliyekuwa akitolewa macho na Simba, amejiunga na Yanga kwa mkataba wa miaka miwili mpaka mwaka 2015.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC