Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HASSANOO SASA JELA INAMUITA

Shahidi Solomon Makogo ambaye ni Afisa Utumishi wa Kampuni ya Liberty Express ameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutunamna wizi wa shaba wenye thamani ya Sh. milioni 400 ulivyofanyika katika kesi inayomkabili katibu wa zamani wa Simba na mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA), Hassan Hassanol 'Hassanoo' (43)  (Pichani) pamoja na wenzake watatu.

Makogo alitoa ushahidi wake jana mbele ya Hakimu Devotha Kisoka. Mawakili wa upande wa Jamhuri waliongozwa na wakili mwandamizi wa serikali, Tumaini Kweka huku upande wa utetezi ukiongozwa na mawakili Richard Rweyongeza na Majura Magafu.

Shahidi huyo alidai kuwa siku ya tukio alipigiwa simu na Rahimu Jeta ambaye ni mkurugenzi wake na kuambiwa kwamba kuna gari lililotoka Zambia kuja Dar es Salaam linaonekana limepaki pembeni ya barabara na lilikuwa wazi bila mizigo.

Shahidi huyo alidai kwamba alikuwa ameongozana na dereva wa gari lake, Abdalah Kota na wakaenda kituo cha polisi kuomba kuongozana hadi katika mahala lilipokuwa gari hilo aina ya Scania lenye namba T821 DCL.

Alidai kwamba alipigiwa simu na Jeta aende kuripoti Kituo cha Polisi Oysterbay na baada ya hapo wakaongozana na polisi hadi Bahari Beach, kwenye Yard ya Najim na kukuta madini ya shaba yaliyokuwa yakitoka Zambia kuja Tanzania huku yakiwa yamefunikwa turubai jekundu.

Aliieleza mahakama kuwa waliangalia kwenye mfumo wa ufuatiliaji kwa njia ya kompyuta, na kuona gari lilifika jijini usiku na kuelekea hadi eneo hilo ambalo shaba hiyo ilipelekwa badala ya bandari kavu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC