Ruka hadi kwenye maudhui makuu

GOR MAHIA YAZIDI KUPETA KENYA

Teddy Akumu 

Gor Mahia walipanua pengo kati yao na wapinzani wao kileleni mwa Ligi Kuu ya Kenya kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Karuturi Sports kwenye mechi iliyochezewa uwanja wa City mnamo Jumamosi.

Mechi hiyo ilianza kwa mwendo wa kasi sana ikihusisha timu iliyo juu ligini na iliyo chini.
Paul Mungai Kiongera na Innocent Mutiso ndio waliotamba zaidi upande wa Gor Mahia kipindi cha kwanza na walifanikiwa kutumia kasi ya mchezo kufanya mashambulio makali upande wa Karuturi.
Mashambulio hayo yaliumiza Karuturi dakika ya tatu huku Samuel Kariuki akiadhibiwa na refa kwa kumchezea visivyo Erick Ochieng’.
Joseph Njuguna alipoteza nafasi ya mwaka huku kombora lake likiokolewa na Ayuko kwa kutumia miguu yake kunako dakika ya 12.
Gor walijipata kifua mbele dakika ya 17 baada ya Omondi kutuma wavuni mpira ulioandaliwa na Kiongera ambaye alikuwa amempokonya mpira Emmanuel Olupot.
Karuturi, hata hivyo, walijikwamua na wakaanza kufufuka kupitia kasi ya John Kiplangat aliyeshirikiana vyema na kifaa kutoka Uganda Zzinda Hussein.
Fowadi huyo wa zamani wa Gor, Kiplangat, alifanya mambo dakika ya 32 – na kumlazimisha kipa Jerim Onyango kufanya kazi ya ziada kuokoa kombora lake upande wa kulia.
Jeraha lililompata Eric Ochieng, hata hivyo lilimlazimisha kocha Bobby Williamson kufanya badiliko lake la kwanza huku difenda kutoka Uganda Ivan Anguyo akiingia uwanjani.
Kipindi cha pili kilikuwa na visa zaidi kwani kila upande ulijizatiti kudhibiti mchezo, lengo likiwa kufunga mabao. Karuturi hapo walifunga bao lililoonekana kuwa la utata na kusawazisha kupitia kifaa kutoka Uganda Zzinda Hussein kunako dakika ya 50 baada yake kuonekana kana kwamba alikuwa ameotea.
Zzinda alituliza mpira kwa kutumia kifua eneo la hatari na kisha akautuma nyuma ya Jerim Onyango aliyekuwa akimkaribia.
Mchezo ulisimamisha karibu dakika tano baada ya wachezaji wa Gor Mahia kulalamikia hatua ya refa mkuu na mtunza mstari ya kuruhusu bao hilo lakini lilibaki.
Gor baadaye waliwatia presha Karuturi baada ya mchezo kuanza huku mafowadi wake wakifanya mashambulio makali na kuwafanya mashabiki wa Karuturi wakose kutulia kwenye viti vyao.
Israel Emuge baadaye aliwarejeshea Gor Mahia uongozi kunako dakika ya 70, kwa kufunga mpira wa kichwa kutoka kwa mkwaju wa adhabu uliotwangwa na Innocent Mutiso ambao ulikuwa umesababisha mtafaruku karibu na goli.
Karuturi hawakuweza kujikwamua licha ya refa kuongeza dakika nane za ziada kwani Gor walikwamilia uongozi na wakasonga hadi alama saba mbele ya Thika United kwenye jedwali.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC