Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AZAM YAIENDEA YANGA 'SAUZI' AGOSTI 2

SHIRIKISHO la soka Tanzania (TFF) limebariki ziara ya Azam FC (Wakiwa pichani) nchini Afrika Kusini kujifua kwa wiki mbili kabla ya kurejea tayari kwa msimu mpya wa Ligi Kuu itakayoanza Agosti 24.


Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Klabu hiyo, Idrisa Nassoro, Azam itakayoondoka Agosti 2, itacheza mechi tatu za kirafiki ambapo baada ya kurejea itacheza mechi ya Ngao ya Hisani Agosti 17, ikiwa ni ufunguzi wa msimu mpya.

Nassoro alisema, maandalizi ya safari hiyo yamekamilika kwani wachezaji wote wako tayari isipokuwa wachezaji wawili Brian Umonyi na Anfrey Mieno ambao watabaki kutokana na kuwa majeruhi.

“Kila kitu kimekamilika; tumebakia kuondoka tu. TFF wana taarifa juu ya safari yetu. Umonyi anasumbuliwa na maumivu ya msuli huku Mieno akiwa na maumivu ya kifundo cha mguu,” alisema Nassoro.

Alisema kukawia kwa safari yao ilikuwa ni kusubiri uhakika wa tarehe ya kuanza kwa Ligi Kuu pia baadhi ya nyota wao kuwemo kwenye kikosi cha timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, inayokabiliwa na mechi dhidi ya Uganda itakayochezwa mwishoni mwa wiki hii mjini Kampala.

Akizungumzia ziara hiyo, Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah, alikiri kupata barua ya ziara ya Azam na kuwatakia kila la kheri katika ziara hiyo kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu.

Mbali ya Ligi Kuu ya bara, Azam chini ya kocha wake Stewart Hall, inakabiliwa na michuano ya Kombe la Shirikisho kama ilivyokuwa msimu uliopita ambapo licha ya kucheza mara ya kwanza, ilifika hadi raundi ya pili iking’olewa na FAR Rabat ya Morocco.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC