Ruka hadi kwenye maudhui makuu

YANGA YAMALIZA KUSAJILI, YABARIKI KUMTOSA KIIZA

Klabu ya Yanga imesema imefunga usajili wa wachezaji wazawa, siku mbili baada ya kumchukua mlinda mlango Deogratias Munishi 'Dida' kutoka timu ya Azam.

Akizungumza  jana, Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Yanga Abdallah bin Kleb alisema wamefanyia kazi mapendekezo ya kocha Ernest Brandts juu ya wachezaji wazawa aliokuwa akitaka kuwaongeza kwenye kikosi chake kwa ajili ya msimu ujao.

Bin Kleb alisema usajili wa mlinda mlango huyo ambaye amewahi kuzichezea Simba kabla ya kuhamia Azam, ulipendekezwa na Brandts baada ya kuachana na mpango wa kumsajili kipa wa zamani Mghana, Yaw Berko.

"Usajili wetu umefanyika baada ya mapendekezo ya kocha wetu... ni yeye aliyetaka tumsajili Dida na tumefanya hivyo," alisema Bin Kleb.

Aidha, alisema baada ya Dida hakuna nafasi ya mchezaji wa ndani kwa kuwa tayari wamemaliza kufanyia kazi mapendekezo ya Brandts kwa upande wa wazawa.
Alisema wataongeza mchezaji mwingine mmoja kutoka nje ya nchi bila ya kumtaja mchezaji huyo wala nchi anayotokea.

"Siwezi kukuambia kitu ambacho hatujakikamilisha," alisema Bin Kleb ambaye kamati yake ilifanya usajili mzuri ulioongeza rekodi kwa kuipa ubingwa wa 23 wa Bara msimu uliopita na kuelekea kurudia jambo hilo tena katika dirisha hili.

"Tupo kwenye mazungumzo na mchezaji wa nje ya nchi na mambo yakiwa tayari tutaweka wazi kama ilivyokawaida yetu."

Hata hivyo, taarifa zilizozagaa ni kuwa Yanga ipo kwenye mbio za kumsajili mshambuliaji wa Uganda anayewaniwa pia na Simba, Moses Oloya anayecheza soka nchini Vietnam.

Yanga inaendelea kusajili mchezaji wa ziada wa kigeni baada ya shirikisho la soka, TFF, kuahirisha hadi msimu ujao kuanza kutumika kipengele cha Azimio la Bagamoyo la mwaka 2010 ambacho kinataka timu zisisajili zaidi ya wachezaji watatu wa kigeni.

Yanga imeshawasajili Haruna Niyonzima (Rwanda), Didier Kavumbagu (Burundi) na Mbuyu Twite (JK Kongo) kutoka nje ya nchi mpaka sasa.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC