Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Yanga kutembeza kombe mikoani

Baraka Kizuguto
Mabingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Yanga watafanya  ziara ya mikoa kadhaa nchini kutembeza kombe lao la ubingwa wa ligi hiyo msimu uliopita kuanzia Julai 5, imeelezwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Afisa Habari wa klabu hiyo, Baraka Kizuguto alisema kikosi chao kinachonolewa na kocha Mholanzi Ernie Brandts kitatua jijini Mwanza Julai 5 kuanza ziara hiyo ambayo pia wataitumia kwa kucheza mechi za kirafiki kujiandaa kwa msimu ujao.

Kizuguto alisema wakiwa Kanda ya Ziwa, kikosi chao kitacheza mechi dhidi ya mabingwa wa Ligi Kuu ya Uganda, timu ya Kampala City Council (KCC), Julai 6 kwenye Uwanja wa CCM Kirumba (Mwanza), Julai 7 kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga na Julai 11 watavaana tena na Waganda hao kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.

“Lengo la ziara hii ni kuwashukuru mashabiki kwa kuiunga mkono klabu na kupata mazoezi kabla ya msimu mpya,” alisema Frank Pangani, Mkurugenzi Mwendeshaji wa kampuni ya Nationalwide, ambao ndiyo waandaaji wa ziara hiyo.

Msimu uliopita Yanga walitwaa ubingwa kwa kishindo baada ya kumaliza kileleni mwa msimamo wa mwisho wa ligi wakiwa na pointi 60, nne zaidi ya Azam waliowafuatia katika nfasai ya pili huku mahasimu wao wa jadi, Simba wakishika nafasi ya tatu wakiwa na pointi 45.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Beno Ngassa mdogo wa Mrisho Ngassa anayekipiga Tanzania Prisons

Miongoni mwa viungo wa pembeni wanaofanya vizuri ni Benodict Khalfan Ngassa ambaye amekuwa akifanya vizuri. Ngassa ambaye ni mtoto wa mchezaji wa zamani wa Pamba Jiji na Simba SC, Khalfan Ngassa, pia ni mdogo wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Simba na Azam, Mrisho Ngassa anatajwa ni mmoja kati ya wachezaji wanaotazamiwa kufanya makubwa siku za usoni. Mambo Uwanjani Blog itawaletea Makala maalum ya kiungo huyo hatari ambaye ndoto zake ni kufuata nyayo za kaka yake Mrisho Ngassa. Beno Ngassa