Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tenga: Wachezaji lazima wapimwe


Leodegar Tenga imesema kuna kanuni inayozitaka klabu za Ligi Kuu kuwapima afya wachezaji inaowasajili na kwamba, kinyume na hatua ni kosa.


Klabu za Ligi Kuu Bara zimeendelea kufanya usajili wa wachezaji bila kuwapima afya kama taratibu zinavyotaka, na kwa hali hiyo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema litaliangalia suala hilo kwa uzito mkubwa.
Kanuni za usajili kama zilivyoainishwa na TFF, inazitaka klabu kuhakikisha zinawapima afya wachezaji wapya wanaowasajili kabla ya kuanza kucheza, jambo ambalo ni kinyume na timu nyingi. Rais wa TFF, Leodegar Tenga alisema jana kuanzia mwaka ujao, hakuna klabu itakayoruhusiwa kusajili wachezaji wapya bila kwanza kuwapima afya na hiyo ni kwa mujibu wa kanuni.
Tenga alisema kanuni ziko wazi kwamba, mchezaji ni lazima apimwe afya kabla ya kusajiliwa, na hii iko kila sehemu mchezo wa soka unakochezwa kwa kiwango cha juu.
“Kuanzia mwaka ujao, TFF haitapokea mikataba ya usajili wa wachezaji  ambayo haitaambatana na taarifa za afya ya mchezaji baada ya kupimwa na klabu anayokwenda kujiunga.
“Kupima afya ya mchezaji kabla ya kumsainisha mkataba ni suala la kikanuni, siyo suala la hiyari na TFF kwa upande wake itahakikisha zoezi hilo linafanyika,” alisema Tenga.
“Kuna mambo mengi yanafanyika kiholela, TFF imejitahidi kwa uwezo wake kuyashughulikia kama msimamizi wa soka,” alisema. Aliongeza: “Tumeanza kutekeleza kwa vitendo kanuni moja baada ya  nyingine na ndiyo maana msimu uliopita tulizibana klabu kuhusu timu B kucheza ligi na hilo lilifanyika.
“Tunafahamu kuna ugumu, hayawezi kutekelezeka yote kwa mara moja lakini tunamaliza moja na kuchukua lingine hadi mpaka tutakapoona klabu  zinaendeshwa kisasa.”
Akizungumzia suala hilo, Meneja Wa Azam FC, Patrick Kahemele alisema  kwa utaratibu wa klabu yao ni lazima wachezaji wa wageni wapimwe afya  zao kabla ya kusajiliwa ndani ya timu.
“Hatujawahi kusajili mchezaji bila kumpima afya, labda awe mchezaji wa  ndani ya timu kwa maana ya kumpandisha daraja kwa sababu wao tayari  wanakuwa wamepimwa,” alisema Kahemele.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...