Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA YALIPIZA KISASI YANGA, YAFANYA USAJILI KIMAFIA

Wakati uongozi wa klabu ya Yanga ukiwa katika harakati za kutaka kumsajili Mganda Moses Oloya anayecheza soka nchini Vietnam, uongozi wa Simba ambayo pia inamuwania mshambuliaji huyo umesema utawapiga bao watani wa jadi wao hao.

Akizungumza  kwa njia ya simu akiwa Nairobi, Kenya Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba, Zacharia Hanspope alisema jana kuwa wanajua kuwa Yanga wanamfuatilia mchezaji huyo lakini hawatishiki.
Alisema hawatishiki kwa kuwa wamefikia hatua nzuri ya mzungumzo na mchezaji huyo anayemalizia mkataba wake kwenye klabu yake ya huko Vietnam.
Hanspope alisema Simba haishindani na timu yoyote katika usajili na kwamba inafuata matakwa ya benchi la ufundi.
"Ni kweli sisi tunamfuatilia huyo mchezaji na bado tupo naye kwenye mazungumzo ila kwa kiasi kikubwa tumekubaliana vitu vingi," alisema mwenyekiti huyo.
"Kwa sasa kuna jambo moja tu tunalolisubiri ili kukamilisha taratibu zote."
Yanga imezoea kuingilia kati kila usajili unaofanywa na Simba, alisema Hanspope, lakini safari hii timu yake ipo makini kutorudia makosa waliyoyafanya msimu uliopita.
Simba iliporwa beki Mbuyu Twite wa APR wakati huo licha ya kuwa ya kwanza kufanya naye mazungumzo, na mwenyekiti Isamil Aden Rage kupiga naye picha nchini Rwanda, baada ya Yanga kwenda kwa klabu mama ya mchezaji huyo ya FC Lupopo ya JK Kongo.
Alisema kuwa suala la usajili wa Oloya wanaliendesha kwa umakini mkubwa kwa kuwa wanafahamu wenzao wanaweza wakawatibulia na kushindwa kukamilisha usajili huo.
Wakati Hanspope akisema hivyo, Yanga wanaendelea kusaka mchezaji mmoja wa kimataifa na taarifa zilizopo ni kuwa yupo kiongozi aliyekwenda Vietnam kwa ajili ya kufanya mazungumzo na kumalizana na mchezaji huyo.
Hata hivyo Mwenyekiti wa Kamati ya usajili ya klabu hiyo Abdallah bin Kleb alikataa kuzungumzia jambo hilo na kusema,
"Sitaki kuzungumzia jambo hilo kwa sasa mpaka hapo mambo yatakapokamilika ila tunatafuta mshambuliaji mmoja wa kimataifa," alisema bin Kleb.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC