Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Simba yafanya kufuru, Yasajili watatu kwa mpigo

Katika kuhakikisha haifanyi makosa zaidi, klabu ya Simba juzi iliwasainisha wachezaji watatu, Sino Agustino, Marcel Kaheza ‘Rivaldo’ na Omary Salum ‘Inzagi’.

Sino ni mshambuliaji amesajiliwa na Simba akitokea Prisons ya Mbeya kwa mkataba wa miaka miwili, ambapo mshambuliaji Malceli na beki wa kushoto Omary wamepandishwa kutoka Simba B.
mtanda huu uliwashuhudia wachezaji hao wakisaini kwenye ofisi za Kaimu Mwenyekiti wa Simba, Joseph Itang’are ‘Kinesi’ Sinza jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia usajili huo, Itang’are alisema,”Katika kuhakikisha hatufanyi makosa tumemalizana na wachezaji hawa kwa lengo la kuiboresha timu katika msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.”
Alisema,”Tumewasajili vijana hawa baada ya kufanya majaribio na makocha wameridhika na viwango vyao kwa kipindi chote cha majaribio,”alisema Itang’are.
Naye, Sino akizungumzia kusajiliwa na Simba alisema amefurahishwa na benchi la ufundi la Simba kwa kumwamini na kumjumuisha kikosini hapo, hivyo ameahidi kuifanyia kazi nzuri klabu hiyo ya mtaa wa Msimbazi.
“Nashukuru kuchaguliwa Simba, nawaahidi mashabiki nitawafanyia kazi nzuri, kikubwa naomba ushirikiano wao,”alisema Sino.
Naye Malcel alisema,” Nimefurahi kusajiliwa Simba na sasa najipanga kuhakikisha naifanyia mazuri klabu hii kwenye ligi na mashindano mengine yatakayotukabiri.”
Kwa upande wa Omary yeye alisema atajitoa kwa nguvu zote kuifanya Simba ing’are.  
Tayari Simba imempa mkataba tena Amri Kiemba, imemsajili beki Samwel Senkoon raia wa Uganda kutoka URA, imemsajili Andrew Ntala kutoka Kagera Sugar, Ibrahim Twaha ‘Messi’ kutoka Coastal Union ya Tanga na wengine wa timu B kama Ramadhani Singano ‘Messi’, Hassan Khatib na Edward Christopher.
Katika hatua nyingine, Simba iliifunga timu ya Kiluvya bao 1-0 katika mechi ya kirafiki iliyochezwa juzi kwenye Uwanja wa Kinesi jijini Dar es Salaam.
Bao hilo la Simba lilifungwa na Sino kutokana na pasi ya Malcel.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC