Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA KUTANGAZA KIKOSI CHAKE LEO, TALIB HILAL AISHANGAA SIMBA KUMTEMA KASEJA

Evodius Mtawala
 
Hatimae kikosi cha 'Wekundu wa Msimbazi', Simba kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara utakaoanza Agosti 24 kitajulikana leo wakati kamati ya utendaji ya klabu hiyo itakapokutana jijini Dar es Salaam chini ya mwenyekiti wake Ismail Aden Rage.

Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo imeeleza kuwa Rage na wenzake watapokea orodha ya majina ya wachezaji yaliyopendekezwa na benchi la ufundi la timu yao linaloongozwa na kocha Abdallah Kibaden ili kuyapitisha.

Akizungumza na gazeti hili jana, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, alisema kuwa kikao hicho kitahudhuriwa pia na Kibaden ambaye ndiye atakayewasilisha majina ya wachezaji atakaowatumia msimu ujao.

Mtawala alisema kuwa kabla ya kufikia maamuzi ya kupitisha wachezaji, Kibaden atatakiwa kuwasilisha maelezo ya kiufundi ya kila mchezaji aliyemtaja kwenye orodha yake hiyo.

"Ilikuwa tukutane jana (Alhamisi), lakini wajumbe wengi walitoa udhuru na hivyo kuamua kuahirisha kikao hicho muhimu," alisema Mtawala.

Aliongeza kwamba kabla ya kikao cha leo, wajumbe wa kamati hiyo ya utendaji walipata nafasi ya kwenda kwenye mazoezi na kuona uwezo wa wachezaji hao ili watakaokutana wafanye maamuzi ya kuijenga Simba.

"Kikao kitakuwa na agenda moja tu, mengine yanayohitaji ufumbuzi yatafanyiwa kazi siku nyingine," aliongeza.

Habari kutoka ndani ya klabu hiyo zimeeleza kuwa katika kikao kilichopita, wajumbe waliamua kufanya maamuzi ya usajili wa kipa Juma Kaseja kwa kupiga kura na inadaiwa ni wawili ndiyo waliompigia kura kipa huyo aliyeitumikia Simba tangu mwaka 2002 akitokea Moro United ya Morogoro.

Wakati huo huo, aliyekuwa kocha mkuu na mchezaji wa timu hiyo, Talib Hilal, ameibuka na kuyoa maoni yake kuhusiana na Kaseja kwa kusema kuwa kipa huyo chaguo la kwanza la Simba hastahili kuachwa katika kikosi cha timu hiyo msimu ujao.

Akizungumza  kwa njia ya simu kutoka Muscat, Oman, Talib, ambaye kwa vipindi tofauti hurejea nchini na kuisaidia Simba, alisema kwamba  timu hiyo ilipaswa kujihakikishia kuwa na kipa mbadala kabla ya kufanya maamuzi ya kumtema Kaseja.

Talib alisema kwamba Kaseja bado ana uwezo wa kuisaidia timu na ili awe bora anatakiwa kupata mabeki wenye uzoefu na wanaojua kujipanga.
"Sikubaliani na bado sijaona kipa aliyeandaliwa, unataka kumuacha mtu wakati kiraka wake hujui atatokea upande gani. Kaseja anastahili na ndiyo maana ni Tanzania One," alisema Talib.

Hadi sasa, Simba ina makipa wawili ambao ni Mganda Abel Dhaira na Andrew Ntalla aliyetua Msimbazi hivi karibuni akitokea Kagera Sugar.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC