Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Simba bado yamng'ang'ania Juma Kaseja


Juma Kaseja
 
Uongozi wa klabu ya Simba umekanusha kumtosa kipa wao chaguo la kwanza Juma Kaseja na kusisitiza kuwa bado nahodha huyo wa timu ya taifa (Taifa Stars) bado anayo nafasi ya kupewa mkataba mpya wa kuendelea kuichezea timu hiyo katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara utakaonza Agosti 24.

Kaseja aliyejiunga na Simba mwaka 2002 akitokea Moro United ya Morogoro, anamaliza mkataba wake wa kuitumikia klabu hiyo Jumapili ya Juni 30 mwaka huu.

Akizungumza na gazeti hili, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, alisema kwamba suala la Kaseja bado liko mikononi mwa viongozi wa klabu hiyo na maamuzi yoyote yanaweza kufanyika ndani ya mwisho wa wiki.

Mtawala alisema kwamba kiufundi, Kaseja anakubalika lakini nje ya uwanja ndiyo kuna maneno 'yanayommaliza' kipa huyo ambaye pia ni nahodha wa klabu yao.

"Kiufundi huwezi kumuacha Kaseja kirahisi. Lakini kuna mambo mengi yanazunguka katika usajili wake na hivyo ni lazima watu wakutane na kujadiliana kwa hoja kabla ya kufikia muafaka, ila bado kikao cha mwisho hakijafanyika na hivyo binafsi siwezi kusema kama atakuwapo au hatakuwapo msimu ujao," aliongeza Mtawala.

Alisema kwamba pamoja na lawama anazopewa kipa huyo na baadhi ya mashabiki, ukweli unabaki kwamba kwa ujumla wake, bado ni kipa hodari na amekuwa akikubali kuitumikia timu hata pale ambapo hakuwa ametarajia kuanza kutokana na sababu mbalimbali zinazojitokeza kwenye kikosi.

"Tofauti na timu nyingine makipa wengi wanadaiwa kutopendana, kwa Kaseja na Dhaira wao hiyo ilikuwa tofauti, wanashauriana na kuzungumza mara kwa mara," alisema Mtawala.

Simba ilimaliza msimu uliopita ikiwa katika nafasi ya tatu hivyo mwakani haitashiriki mashindano yoyote ya kimataifa.
Kocha wa klabu hiyo, Abdallah Kibaden 'King' aliumbia mtandao huu hili hivi karibuni kuwa si yeye aliyemtema Kaseja bali viongozi wa klabu hiyo ndiyo wanajua siri ya sababu ya kuliondoa jina la kipa huyo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC