Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Serikali yakosa mwendeshaji Uwanja wa Taifa

Leonard Thadeo
Serikali bado haijapata kampuni inayokidhi vigezo ili kuingia nayo ubia wa kuendesha Uwanja wa Taifa uliopo jijini Dar es Salaam, imeelezwa.

Akizungumza kwenye ofisi za makao makuu ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo, Leonard Thadeo alisema kuwa bado wanaendelea kusaka kampuni ya kuendesha uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watu 57,558.

"Bado tunaendelea na mchakato wa kutafuta mtu au kampuni yenye uwezo wa kuendesha uwanja wetu, tukishakamilisha tutawajulisha," alisema Thadeo bila kutaja kampuni ambazo tayari zimeshajitokeza kuomba zabuni hiyo.

Mkurugenzi Msaidizi wa Maendeleo ya Michezo, Juliana Yassoda naye hakutaka kuweka wazi kampuni zilizochangamkia zabuni hiyo huku akisema kuwa kuna kampuni nyingi ambazo zimekuwa zikijitokeza lakini hawajaipata yenye sifa wanazozihitaji.

"Wengi wamejitokeza tangu tulipotangaza tenda hiyo lakini bado hatujapata kampuni sahihi ya kuuendesha. Wengine wanakuja, tunaongea nao lakini wanaenda na hawarudi tena kuendelea na mazungumzo," alisema Yassoda.

Serikali kupitia wizara yenye dhamana ya michezo nchini imekuwa ikitoa matangazo ya kusaka kampuni kwa ajili ya kuuendesha uwanja huo pindi tu kampuni ya Beijing Construction ya China itakapoukabidhi kwa serikali
ilianza kujenga Uwanja wa Taifa mwaka 2005 lakini hadi sasa bado haijaukabidhi rasmi kwa serikali.

Februari 15, 2009 Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, Hu Jintao, aliyekuwa amefuatana na mwenyeji wake Rais Jakaya Kikwete, aliuzindua rasmi uwanja huo.

Kila mechi ya klabu na timu za taifa inayochezwa katika uwanja huo, serikali hupata asilimia 15 ya mapato baada ya makato ya kodi, mbali na ingizo jingine kupitia makato mbalimbali yakiwamo ya Kodi la Ongezeko la Thamani  (VAT).

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC