Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Profesa Jay, Jide wang'ara tena tuzo za Kill

Lady Jaydee, ambaye anashikilia tuzo ya mwanamuziki bora wa kike, akipagawisha mashabiki wakati wa uzinduzi wa ziara ya kimuziki ya Kili kwenye uwanja wa Jamhuri Mkoani Dodoma, juzi Jumamosi.
Ziara ya mikoa 10 ya kimuziki yenye lengo la kuupa nguvu muziki wa Kitanzania na utamaduni wake kwa ujumla, ilianza juzi katika viwanja vya Jamhuri mkoani Dodoma na kujumuisha wanamuziki saba wanaong'ara katika tasnia ya muziki Tanzania huku wakongwe na chipukizi wakitoana jasho.
Ziara hiyo iliyodhaminiwa na kampuni ya bia ya TBL kupitia kinywaji chake cha Kilimanjaro, ilijumuisha wanamuziki mchanganyiko kama Judith Wambura, Linex Sunday, Roma Mkatoliki, Ommy Dimpoz, Kala Jeremiah, Profesa Jay na mkali wa muziki wa R&B nchini Ben Pol.
Wanamuziki waliotia fora katika tamasha hilo ambalo wiki ijayo linatarajia kuelekea katika mkoa wa Tanga ni Ben Pol ambaye alikuwa wa pili kupanda jukwaani. Mashabiki walionekana dhahiri kumuelewa na kuitikia kila wimbo aliokuwa akiimba na kusababisha wakati mwingine yeye kukaa kimya na kuachia mashabiki hao waimbe mwanzo hadi mwisho wa wimbo.
 
Ben Pol alipanda na wimbo 'Maneno Maneno' na kusababisha shangwe kubwa uwanjani, na baada ya hapo, aliimba nyimbo zake maarufu kama 'Pete', 'Jikubali', 'Samboira', 'Nikikupata' na 'Maumivu'.
 
Lady Jaydee alikuwa ni mwanamuziki mwingine aliyeshangiliwa sana, baada ya kupanda jukwaani akiwa bila bendi, jukwaa ambalo aliacha kupanda kwa takriban miaka saba sasa, mara baada ya kuanzisha bendi yake ya Machozi.
 
Jaydee alipanda jukwaani na wimbo aliomshirikisha marehemu Albert Mangweha, ambapo baada ya kumaliza alisema ni heshima yake kwa kijana huyo ambaye ameacha alama katika muziki wa kizazi kipya nchini. Baada ya hapo aliendelea na vibao kama 'Wangu', ambapo alikuwa akiimba na kurap mwenyewe, hali iliyosababisha uwanja mzima wa Jamhuri kushangilia muda wote aliokuwa akiimba.
 
Ulipofikia wakati wa kuimba wimbo wa 'Joto Hasira', akasindikizwa na Profesa Jay ambaye alizidi kupagawisha maelfu ya wakazi wa Dodoma waliokuwa wamefurika uwanjani hapo kuangalia uzinduzi wa ziara hiyo ya muziki ya Kili ambayo mwaka huu haijumuishi washindi wa tuzo kama ilivyo kawaida, bali wasanii wanaong'ara katika medani ya muziki wa kizazi kipya.
 
Akiongea baada ya onesho hilo, Meneja wa Bia ya Kilimanjaro, ambaye alionekana kufurahia onyesho alifafanua kwamba kampuni yake, kupitia bia ya Kilimanjaro imedhamiria kuupeleka muziki wa Tanzania katika hadhi yake na ndio maana mwaka huu, imebeba mandhari ya kikwetukwetu, ili kuipa sanaa ya Kitanzania nafasi ya kutambulika.
 
Ziara hiyo inatarajia kuendelea wiki ijayo katika mkoa wa Tanga kabla ya kuelekea Moshi wiki inayofuata

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC