Ruka hadi kwenye maudhui makuu

PELLEGRINI AMTAKA FRED WA BRAZIL

Premier player: Brazil's Fred (left) is a target for Manchester CityKOCHA wa Manchester City, Manuel Pellegrini amehamishia mawindo yake kwa washambuliaji Mbrazil, Fred na Oscar Cardozo wa Benfica, baada ya kuamua kuachana na Edinson Cavani aliyekuwa anatakiwa na kocha aliyemtangulia, Roberto Mancini aliyetimuliwa.

Pellegrini, ambaye amepewa kauli ya mwisho kuhusu usajili katika klabu hiyo licha ya kuwepo kwa Mkurugenzi wa Soka, Txiki Begiristain, hataki City ibomoe benki kwa ajili ya Cavani, baada ya klabu yake, Napoli kukataa ofa iliyotolewa ya Pauni Milioni 54. 

City bound: Oscar Cardozo could be a ready replacement for Carlos Tevez
Anayewatoa udenda City: Oscar Cardozo anaweza kuchukua nafasi ya Carlos Tevez
 
Mshambuliaji wa Fluminense, Fred, ambaye ataiongoza nchi yake leo katika Fainali ya Kombe la Mabara dhidi ya Hispania, kwa sasa anatabirwa kwenda kuziba pengo la Carlos Tevez, aliyejiunga na Juventus wiki iliyopita. 
Fred, mwenye umri wa miaka 29, alifunga wakati Brazil inatoa sare ya 2-2 na England mapema mwezi huu na akafunga mabao mawili dhidi ya Italia katika michuano hii ya kupashia misuli moto Kombe la Dunia inayofikia tamati leo. 
Cardozo, mshambuliaji wa Montenegro, Stevan Jovetic na Stephan El Shaarawy, wa AC Milan, pia wametajwa kama wawania kurithi mikoba ya Tevez huku Pellegrini akitarajia kutengeneza alama yake katika klabu hiyo kabla hajaanza mazoezi ya kujiandaaa na msimu mpya. 
Kwa muda mrefu, Mancini alimfanya mshambuliaji wa Uruguay, Cavani chaguo la kwanza katika wachezaji anaowataka, lakini akafukuzwa City siku kadhaa baada ya kufungwa kwenye Fainali ya Kombe la FA na Wigan mwezi uliopita.
Pellegrini, ambaye aliiongoza Malaga kutinga Robo Fainali za Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita, anataka kuongeza mshambuliaji na na sentahafu, baada ya kukamilika kwa usajili wa winga wa Hispania, Jesus Navas na kiungo wa Brazil, Fernandinho. 
City inataka kukata Pauni Milioni 20 kumnunua beki wa kati wa Real Madrid, Pepe, ambaye atatengeneza ushirikiano mpya na Vincent Kompany.
Mpango wao wa sasa kutaka kumsajili Pepe ni pigo kubwa kwa beki wa sasa wa City, Joleon Lescott, ambaye anatarajia kuwa na mazungumzo na klabu hivi karibuni juu ya mustakabali wake.
Lescott, mwenye umri wa miaka 31, anataka uhakika wa namba katika kikosi cha kwanza, ili kulinda nafasi yake katika kikosi cha timu ya taifa ya England, kuelekea Fainali za Kombe la Dunia mwakani, Brazil.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC