Ruka hadi kwenye maudhui makuu

NEYMAR: HATUIHOFII HISPANIA

NYOTA wa Brazil, Neymar anaamini Hispania inapewa nafasi kubwa ya kutwaa Kombe la Mabara katika Fainali itakayopigwa leo usiku, lakini amesema timu yake haiwahofii mabingwa hao wa Ulaya na Dunia.

Hispania inaingia kwenye fainali hiyo leo usiku, ikitazamiwa kushinda taji hilo kwa mara ya kwanza na kuendeleza mafanikio yao ya miaka ya karibuni katika soka, wakitwaa mfululizo mataji ya Euro na Kombe la Dunia.
Mafanikio hayo yameifanya La Roja ishike nafasi ya kwanza katika viwango vya soka duniani na licha ya kwamba Brazil inapewa nafasi kutokana na kucheza nyumbani, Neymar amesema kikosi cha Vicente Del Bosque ni tishio.
Neymar
Mazoezi yanajenga usahihi: Neymar (katikati), ambaye hivi karibuni amesaini Barcelona, akiwa na mpira mguuni mwake

Pamoja na hayo, mshambuliaji huyo ambaye atacheza Ligi Kuu ya Hispania msimu ujao baada ya kujiunga na Barcelona mapema majira haya ya joto, pia ana matumaini na timu yake inaweza kuweka rekodi ya kutwaa kwa mara ya tatu mfululizo Kombe la Mabara na mara ya nne kwa ujumla.
"Wao (Hispania) ni timu nzuri duniani na wanapewa na nafasi,"alisema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21.
"Lazima tucheze soka bila woga. Tunacheza na timu bora duniani kwa sasa, lakini pia tuna wachezaji wazuri katika timu ya taifa ya Brazil,".
Jo and Scolari
Maelekezo: Kocha wa Brazil, Luiz Felipe Scolari (kulia) akizungumza na mshambuliaji wa zamani wa Everton na Man City, Jo

Kocha wa Brazil, Luiz Felipe Scolari amesema kikosi chake kina uwezo wa kuibwaga Hispania.
"Tunacheza na Hispania tukiheshimu ubora wao, lakini pia kujaribu kuonyesha uwezo wetu na vipaji,"alisema.
"Tumefika Fainali na tuna ubora wa kutosha kuwabwaga,".
Nchi hizo mbili zinakutana kwa mara ya kwanza tangu zitoke 0-0 katika mchezo wa kirafiki mjini Vigo mwaka 1999. Mara ya mwisho, Hispania ilipokutana na Brazil Uwanja wa Maracana walifungwa mabao 6-1 - mwaka 1950.
Brazil squad
Samba: (kutoka kushoto) Marcelo, Oscar, Fred, Neymar, David Luiz na Hulk katika mazoezi ya Brazil mjini Rio

Timu zote zimeonyesha ni timu mwaka huu katika Kombe la Mabara, Brazil ikishinda mechi zake zote nne hadi sasa, wakati Hispania walishinda mechi zao zote tatu za kundi lao, kabla ya kuing'oa kwa matuta Italia kwenye Nusu Fainali kali katikati ya wiki.
Andres Iniesta
Andres Iniesta ataiongoza Hispania kesho
Marcelo and Neymar
Wamemaliza siku yao: Nyota wa Real Madrid, Marcelo (kulia) akiburuza kipozeo baada ya mazoezi huku Neymar akimuangalia

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...