Ruka hadi kwenye maudhui makuu

'Mimi bado Tanzania One', Asema Juma Kaseja, Adai ashangazwi kuachwa Simba

 
Kipa aliyefunguliwa mlango kuondoka Mtaa wa Msimbazi, Juma Kaseja amesema taarifa za kutemwa kwake anazisikia kwenye vyombo vya habari tu, na kwamba hata kama ni kweli hazijamshtua kwa vile anaamini kiwango chake bado kimesimama kwenye mstari.

Kwa zaidi ya wiki sasa, vyombo vya habari vimekuwa vikiandika taarifa zilizokosa maelezo ya kina kuhusu kutemwa kipa huyo namba moja wa Simba na nahodha wa timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars.
Kaseja ambaye kwa sasa yuko Kigoma kwa ajili ya mapumziko, alisema anafahamu kuwa mkataba wake na Simba ulishakwisha tangu baada ya kumalizika kwa msimu uliopita, hivyo yeye ni mchezaji huru.
“Nasikia tu nimetemwa Simba, lakini kweli sijapata barua na hata kama ningejulisha, nisingeshangaa kwa sababu mkataba wangu na Simba ulishamalizika,” alisema Kaseja.
Mlinda mlango hiyo mwenye rekodi ya pekee nchini, alisema hana ugomvi na uongozi wa Simba pamoja na kutomjulisha kama hawatamwongezea mkataba.
“Sijawahi hata siku moja kujulishwa kuwa sitaongezewa mkataba mpya baada ya kumalizika uliotangulia. Hakuna kiongozi aliyeniambia lolote zaidi ya kusikia kwenye vyombo vya habari kwamba sitakiwi,” alisema Kaseja.
“Kwa sasa siwezi kuzungumza mengi kwa vile sina haki hiyo kwa sasa, muda utafika nitaongea. Napumzika huku pia nikiendelea kufanya mazoezi kwa sababu soka ndiyo ajira yangu,” aliongeza Kaseja.
Kaseja aliyeidakia Simba kwa miaka tisa mfulilizo tangu mwaka 2003, hakuwa tayari kuweka bayana mwelekeo wake kama uamuzi wa kutemwa Simba utabaki palepale.
Alisema: “Siwezi kusema lolote kwa sasa, ila muda ukifika nitaweka wazi mambo yangu. Naamini bado nina uwezo na kamwe sitakata tamaa hata kama nitaondoka Simba.”
Tangu kutangaza kutemwa kwa Kaseja zaidi ya wiki moja iliyopita, taarifa za ndani kutoka Simba zinadai kuwa uamuzi huo umezaa mgogoro chinichini baina ya viongozi.
Ingawa Mwenyekiti wa Simba Aden Rage, aliwahi kukaririwa akisema kipa huyo hatavaa jezi za Msimbazi msimu ujao, viongozi wenzake wanapinga uamuzi huo.
Kaseja aliwahi kulalamikiwa na mashabiki wa Simba mwishoni mwa msimu uliopita wakimtuhumu kucheza chini ya kiwango hali iliyosababisha kufungwa mabao ya kizembe.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC