Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Ligi Kuu Bara kuanza Agosti 24

Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi, Wallace Karia
 
Msimu mpya wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara 2013/2014 utaanza Agosti 24 mwaka huu ambapo timu zote 14 zitashuka dimbani kwenye viwanja tofauti kusaka pointi tatu muhimu, imefahamika.

Akizungumza jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Ligi, Wallace Karia, alisema kuwa tarehe hiyo imeshapitishwa katika kalenda ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na tayari pia mechi za ligi hiyo zimeshapangwa lakini hazijathibitishwa na kamati yake kama taratibu zinavyoeleza.

Karia alisema kuwa tayari 'wataalamu' ambao huhusika na zoezi la kupanga ratiba za mechi wameshakamilisha zoezi hilo lakini kamati yake ndiyo inasubiriwa kupanga siku ya kukutana ili kuithibitisha.

"Ligi itaanza tarehe 24 Agosti ila nani ataanza na nani ndiyo bado hatujapitisha, tukishakutana na kupitia hilo kwa kuzingatia mazingira yetu ya timu kusafiri ndiyo itatolewa hadharani. Tutakuwa makini sana kwa sababu hatutaki makelele yaliyojitokeza mwaka jana na miaka ya nyuma yaendelee," alisema Karia ambaye ameshasema kuwa atawania cheo cha Makamu wa Rais katika uchaguzi ujao wa shirikisho hilo utakaofanyika Septemba.

Hata hivyo, Karia alisema kuwa suala la wadhamini wa ligi hiyo bado halijakamilika lakini kubwa wanachotaka ni kuona ni klabu zinafaidika na udhamini utakaopatikana.

Alisema kuwa kamati yake inatarajia kukutana Julai 3 asubuhi ili kupitia taarifa za msimu uliopita na kupata washindi wa tuzo mbalimbali na jioni yake washindi hao watatangazwa na kutunukiwa.

"Tumepanga tukutane siku hiyo hiyo ya tuzo ili habari zisivuje, kwa sababu kila mtu na kifua chake cha kuweka mambo…  hadi sasa ni bingwa, mshindi wa pili na wa tatu ndiyo wanajulikana. Lakini kocha bora na tuzo nyingine tutajua siku hiyo baada ya kuangalia na kuthibitisha rekodi tulizonazo," aliongeza Karia.

Kabla ya kuanza kwa ligi hiyo, bingwa mtetezi Yanga na mshindi wa pili, Azam watakutana katika mechi ya kuwania Ngao ya Jamii kama kanuni za ligi zinavyosema.

Timu 14 za msimu ujao wa ligi ni pamoja na Yanga, Azam, Simba, Kagera Sugar, Mtibwa Sugar, Coastal Union, JKT Oljoro, JKT Ruvu, Ruvu Shooting, Mgambo Shooting, Prisons na zilizopanda daraja ambazo ni Mbeya City, Ashanti na Rhino Rangers ya Tabora.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC