Ruka hadi kwenye maudhui makuu

HISPANIA WAING'OA ITALIA KWA MATUTA KOMBE LA MABARA, FAINALI NA BRAZIL MARACANA...NI BALAA

Close shave: Spain moved through to the Confederations Cup final after beating Italy on penalties in FortalezaHISPANIA imeitoa Italia katika Kombe la Mabara kwa ushindi wa matuta wa 7-6 mjini Fortaleza, kufuatia sare ya bila kufungana ndani ya dakika 120 katika mchezo wa Nusu Fainali usiku huu.

Wataliano walifungwa na Waspanyola katika Fainali ya Euro mwaka jana wameshindwa kulipa kisasi na sasa Fainali ya michuano hiyo mwaka huu Jumapili Uwanja wa Maracana, itawakutanisha wenyeji La Roja na Brazil wenyeji.
Leonardo Bonucci wa Italia alikosa moja ya penalti 14 na Jesus Navas akaweka nyavuni mkwaju wa mwisho na kuipeleka Hispania Fainali.


Dramatic: Spain triumphed 7-6 in a dramatic shootout to set up a dream final against Brazil
Ushindi wa mbinde: Hispania wakishangilia 7-6 na sasa watamenyana na Brazil
Heartbreak: Italy were left devastated after pushing the world and European champions the distance
Maumivu: Italia wameng'oka

Si zaidi ya mwaka uliopita, Italia walipigwa 4-0 mjini Kiev, lakini The Azzurri waliwasili Fortaleza wakiamini kisasi kinawezekana, ingawa haikuwa hivyo.
Mikwaju ya penalti;  Jesus Navas alifunga a ushindi na kufanya 7-6 , baada ya Leonardo Bonucci mkwaju wake kuota mbawa.
Wengine wote waliotangulia walifunga; upande wa Hispania ni Sergio Busquets,  Juan Manuel Mata,  Sergio Ramos, Gerard Pique, Andries Iniesta na Hernandez Xavi.
Italia ni Riccardo Montolivo, Andrea Pirlo, Sebastian Giovinco, Daniele De Rossi, Alberto Aquilani na Antonio Candreva.
Kikosi cha Hispania kilikuwa: Casillas, Arbeloa, Sergio Ramos, Pique, Jordi Alba, Xavi, Busquets, Iniesta, Pedro/Mata dk79, Torres/Javi Martinez dk94 na Silva/Jesus Navas dk52.
Italia: Buffon, Maggio, Bonucci, Barzagli/Montolivo dk45,Chiellini, Candreva, De Rossi, Pirlo, Marchisio/Aquilani dk79, Giaccherini na Gilardino/Giovinco dk91.
Off target: Italy blinked first in the shout-out when Leonardo Bonucci fired over at 6-6
Anakosaaa: Leonardo Bonucci mkwaju wake uliota mbawa
Decisive: Jesus Navas stepped up to score the winning penalty and send Spain to the final
Ya ushindi: Jesus Navas alifunga ya mwisho, chini anashangilia
Jesus Navas
Jesus Navas
Glamour: Worldwide superstar Shakira was in the stands in Fortaleza
Shakira alikuwapo jukwaani Fortaleza 
This one is for you: Pique celebrates Spain's victory by the tightest of margins
Hii ni kwa ajili yako: Pique akishangilia ushindi wa Hispania
Support: Shakira was watching her partner Pique in action for Spain 
Shakira jukwaani
Greetings: Shakira meets FIFA president Sepp Blatter in the VIP lounge
Shakira alikutana na Rais wa FIFA, Sepp Blatter katika eneo la VIP uwanjani
Support: Shakira was watching her partner Pique in action for Spain
Shakira akimuangalia mpenzi wake Pique akiichezea HispaniaOn the box: A spectator enjoys the party atmosphere in Fortaleza
Shabiki
Evens: The teams were locked at 0-0 after 120 minutes in the all European semi-final
Dakika 120 ziliisha 0-0 
Outnumbered: Italy's Giorgio Chiellini tries to win a header against Sergio Ramos and Gerard Pique
Giorgio Chiellini wa Italia akijaribu kupiga kichwa katikati ya Sergio Ramos na Gerard Pique
Effort: Fernando Torres attempts a shot on goal as Gianluigi Buffon watches
Jitihada: Fernando Torres alifumua shuti lililopanguliwa Gianluigi Buffon
Stretch: Christian Maggio gets his head to the ball in front of Spanish goalkeeper Iker Casillas
Anateleza: Christian Maggio alikaribia kumtungua kipa wa Hispania, Iker Casillas
On the ball: Manchester City's David Silva attempts one of his elusive runs
David Silva akipasua
Held his nerve: midfielder Andres Iniesta slotted his penalty past Buffon in the Italian goal
Andres Iniesta alimtungua Buffon kwa penalti

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC