Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Hamisi Kiiza ataka kumpiku Niyonzima Yanga

Mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Hamis Kiiza
 
Mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Hamis Kiiza, amesema kwamba yuko tayari kukaa msimu mzima bila ya timu lakini hataweza kushusha kiwango cha mshahara wa mwezi cha Dola za Marekani 3,500 (Sh. milioni 5.6) ambazo anataka mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara wamlipe kuanzia msimu ujao.

Kiiza alikuwa analipwa mshahara wa Dola za Marekani 1,500 kwa mwezi katika misimu miwili aliyoichezea Yanga baada ya kusainiwa kwa kiasi cha Dola za Marekani 30,000 na sasa ameitaka klabu hiyo iliyoutema ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame) impe fedha ya kusaini Dola za Marekani 45,000 (Sh. milioni 72) ili asaini mkataba mpya.

Akizungumza  kwa njia ya simu kutoka kwao Kampala, Uganda, Kiiza alisema kuwa anaamini kiasi hicho cha fedha ndiyo kinalingana na thamani yake kwa sasa.

Mshambuliaji huyo ambaye yupo pia katika kikosi cha timu ya taifa ya Uganda (The Cranes) alisema kuwa mchezo wa soka ndiyo unaoendesha maisha yake na kwa kipindi hiki anatakiwa kufanya maamuzi sahihi ili aweze kujiandaa na maisha baada ya soka.

"Mimi kama nilivyowaambia sijabadilisha kitu, niko tayari hata kutorudi kama hawatakuwa tayari kunilipa, nami pia ninatoa mchango mkubwa kwa timu," alisema Mganda huyo.

Mbali na kiasi hicho cha mshahara ambacho kitakuwa ni cha juu ndani ya Yanga, Kiiza pia ameutaka uongozi umpatie nyumba ya kuishi na gari jipya la kutembelea akiwa hapa nchini.

Kiiza aliongeza kwamba licha ya kutofikia makubaliano na Yanga bado wakala wake hajampatia timu nyingine ya kwenda kufanya majaribio lakini wako kwenye mchakato huo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Abdallah Binkleb, aliliambia gazeti hili jana kwamba wao wako radhi kumuacha nyota huyo kama atashikilia msimamo wake huo.

Binkleb alisema kwamba wanaheshimu maamuzi yake kwa sababu wanajua ni kijana ambaye ana mipango na malengo yake kimaisha ambayo anataka kuyatimiza.

Kikosi cha Yanga kiko kwenye mapumziko na kinatarajia kuanza mazoezi upya Julai 2 mwaka huu kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi utakaofanyika kuanzia Agosti 24.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC