Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CAVANI AWATOSA WAZAZI WAKE, AWAAMBIA WASIMFUATILIE MAISHA YAKE

Wanted man: Cavani is one of Europe's hottest propertiesMSHAMBULIAJI wa Napoli, Edinson Cavani amewapiga stop wazazi wake kuzungumzia mustakabali wake kwenye umma.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 wa Uruguay, alikuwa tayari amehusishwa na mpango wa kuhamia Manchester City, kabla ya mama yake kusema amefanya mazungumzo na klabu zote, City na Real Madrid.
Kisha maelezo ya baba yake yakapendekeza Cavani amekubali kujiunga na Real, kwa dau la Euro Milioni 63 (Pauni Milioni 54).
Hitting out: Cavani trains with his Uruguay team-mates in Brazil on Tuesday
Amewatolea uvivu: Cavani akifanya mazoezi na wachezaji wenzake wa Uruguay nchini Brazil jana
Hitting out: Cavani trains with his Uruguay team-mates in Brazil on Tuesday
Lakini Cavani, ambaye amefunga mabao 29 katika ligi akiwa na Napoli msimu uliopita, amewataka wazazi wake wakae kimya na wakati ukifika utatoa majibu.
Akinukuliwa na La Repubblica, aliwaambia Waandishi wa Habari: "Baba yangu amezungumza kuhusu Real? Nataka niseme hayo maneno si yangu.
"Nimewaambia wazazi wangu mara elfu, wasizungumze tena. Wanaweza kuniumiza tu mimi.
"Mimi ni mali ya Napoli kama ilivyo na hiyo itategemea na klabu. Kama suluhisho lingine, litakuja lenyewe, tutamua.'
Rais wa Napoli, Aurelio De Laurentiis ameripotiwa akisema mshambuliaji wake huyo anatakiwa kufanya uamuzi juu ya mustakabali wake hadi kufikia Julai 20, akirejea kutoka kwenye Kombe la Mabara anakoiwakilisha Uruguay.
Na alipoulizwa ikiwa Real Madrid - ambayo sasa iko chini ya kocha wa zamani wa Chelsea na Paris Saint-Germain, Carlo Ancelotti - itakuwa sehemu yake sahihi, Cavani alibakia kuficha.
"Nitaweka wazi juu ya hilo pia - wakati wote nimekuwa nikisema ni moja ya klabu bora duniani.
Prolific: The Uruguayan was top scorer in Serie A last season
Anatisha: Nyota huyo wa Uruguay amekuwa mfungaji bora wa Serie A msimu uliopita
"Wote tumekuwa tukiota vizuri tu kuchezea timu yao, kama ambavyo tunaota kuhusu Barcelona, lakini sasa nipo Napoli na ninajivunia kwa kweli.
"Kama nitaiacha nyuma jezi ya bluu siku moja, nitajiunga na klabu kubwa tu. Wazi kuna mashabiki ambao wataelewa na wengine ambao hawataelewa.
"Lakini sitaki kuteleza nyuma ya mlango, Nataka kutoka mbele ya mlango, siku ambayo hatimaye mambo yatakuwa,"

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC