Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Blatter atetea FIFA

Sepp Blatter
Rais wa Fifa Sepp Blatter, anaamini kuwa hadhi ya shirikisho la mchezo wa soka duniani imeimarika kutokana na fainali za kombe la shirikisho, inayoendelea nchini Brazil, licha ya maandamano yanayoendelea nchini humo.

Akiongea kwa mara ya kwanza, tangu maandamano hayo kuanza, Blatter amesema anawahurumia raia wa nchi hiyo wanaoandamana katika miji mia moja nchini Brazil.
Maandamano zaidi yanatarajiwa kabla ya fainali za kombe hilo siku ya Jumapili kati ya Brazil na Uhispania katika uwanja wa Marikani mjini Rio.
Kuna wasi wasi mkubwa kuwa huenda rais wa nchi hiyo Dilma Rousseff huenda asihudhuria fainali hiyo.
'' Fifa imekuwa na nguvu zaidi na hadhi yetu imeimarishwa. Mchezo wa soka umekuwa na nafasi kubwa miongoni mwa taifa hili na imewapa fursa ya kuelezea hisia zao'' Alisema Blatter.
Blatter amesema anawahurumia sana raia wa nchi hiyo kwa kuwa anafahamu masuala wanayoyapinga kupitia maandamano hayo ya amani na ameongea kuwa anatarajiwa serikali ya nchi hiyo itatatua masuala hayo kabla ya kuanza kwa fainali ya kombe la dunia itakayoandaliwa nchini humo mwaka ujao.
Maandamano yanayoendelea nchini Brazil
Shirikisho la mchezo wa FIFA limeshutumiwa sana nchini Brazil kwa kupata faida kubwa isiyotozwa ushuru kutokana na fainali za kombe la dunia kuandaliwa nchini humo, na kuiacha taifa hilo kuwekeza mabilioni ya fedha za umma bila manufaa yoyote.
Bwana Blatter hata hivyo amekanusha madai hayo.
''Dhamira kuu ya kombe la dunia sio kupata faida au kuchukua faida yote kutoka kwa nchi inayoandaa mashindano hayo, lakini ni kuisaidia taifa hilo ili kuhakikisha kuwa fainali hizo zinafanikiwa'' Alisema Blatter.
Blatter ambaye aliondoka nchini Brazil wiki iliyopita, huku maandamano hayo yakichacha, amepuuzilia mbali madai kuwa alitoroka Brazil hata bila kuwajulisha maafisa wengine wakuu wa Fifa.
Blatter amesema aliondoka Brazil ili kuhudhuria fainali za kombe la dunia kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 20 inayoandaliwa nchini Uturuki.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC