Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Zana za Hizbollah zapatikana Nigeria

Jeshi lilisema kuwa silaha hizo zilikuwa zimefichwa chini ya vumbi la mbao
Karakana ya silaha inayoaminika kumilikiwa na kundi la Hezbollah, nchini Lebanon imapatikana Kaskazini mwa Nigeria.

Kwa mujibu wa taarifa za jeshi na shirika la ujasusi la Nigeria raia watatu wa Lebanon wamekamatwa. Msemaji wa jeshi, Brigedia Gen Ilyasu Isa Abba, pia amethibitisha hilo.
Silaha hizo ikiwemo, risasi, zana za kukinga magari ya kivita dhidi ya mashambulizi na RPG, zilipatikana ktika karakana mjini Kano.
Maafisa wa usalama walisema kuwa silaha hizo zilinuiwa kutumiwa dhidi ya maslahi ya Israel na nchi za Magharibi.
Hii ni kazi ya Hezbollah," katibu mkuu wa usalama mjini Kano Bassey Ettang alisema.Na unaweza hata kuwa na uhakika kuwa ikiwa hili linafanyika, inawezekana wanasaidia makundi ya kigaidi wanaoendesha harakati zao nchini humu,'' alidokeza bwana Bassey.
Brig Gen Ilyasu Isa Abba alisema kuwa zana 11 za magari ya kivita, guruneti na makombora 21 bunduki 17 aina ya Ak-47 na maguruneti 76 ni baadhi ya silaha zilizopatikana.
Mmiliki wa karakana hiyo, ambako silaha zilipatikana, zikiwa zimefichwa chini ya vumbi la mbao, hakuwa nchini humo.
Kuna jamii kubwa ya walebanese wanaofanya kazi mjini Kano, mji wa kibiashara wa Nigeria Kaskazini.
Mji wa Kano eneo la Kaskazini Mashariki mwa Nigeria zimekubwa na mashambulizi ya mara kwa mara katika miaka mitatu iliyopita, tangu wapiganaji wa kiisilamu Boko Haram walipoanzisha harakati zao.
Bwana Ettang aliongeza kuwa "unaweza pia kuwa na uhakika kundi kama hili likiwa lipo, inaweza hata kuwasaidia wapiganaji wengine walioko nchini humo.''
Hezbollah ni kundi la Kishia pamoja na kuwa vuguvugu la kisiasa lenye makao yake nchini Lebanon. Linatambulika na Marekani kama kundi la kigaidi.
Boko Haram, ambalo jina lake lina maanisha tamaduni za kimagharibi zinapingwa, linasema, nia yake ni kuipindua serikali sasa na kubuni serikali ya kiisilamu.
Kuna wasiwasi mkubwa kuwa kundi la Boko Haram huenda linasaidiwa na mtandao wa kigaidi wa al-Qaeda katika nchi zengine

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC