Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Wabunge wa Kenya wajiongeza mishahara

Wanaharakati nchini Kenya waliandamana kupinga njama ya wabunge kujiongeza mishahara

Wabunge nchini Kenya wamepiga kura kujiongeza mshahara na kwenda kinyume na tume ya kitaifa ya kuratibitisha mishahara ya maafisa wa serikali.

Kura hiyo waliyopiga bungeni hapo Jumanne itawawezesha sasa kupokea mishahara ya dola elfu kumi. Mshahara wa mkenya wa kipato cha kadri ni dola 1,700.
Rais Uhuru Kenyatta aliwaomba wabunge hao mapema mwezi huu kuruhusu mishahara yao kupunguzwa ili waweze kuiwezesha serikali kupata pesa za kutengeza ajira kwa wananchi.
Wabunge wa Kenya ni miongoni mwa wale wanaopokea mishahara mikubwa duniani na hatua yao ya kibinafsi imewaghadhabisha wakenya waliofanya maandamano kuwafananisha wabunge hao na Nguruwe kwa ulafi.
Lakini wabunge hao waliteta kuwa hatua ya kupunguza mishahara yao ni kinyume na sheria.
"wametupokonya utu wetu na lazima tuweze kuurejesha,'' alisema mbunge Jimmy Angwenyi bungeni.
Kura waliyopiga wabunge hao, itapingwa leo mahakamani na makundi ya kutetea haki za binadamu
Rais wa Kenya hana uwezo wa moja kwa moja kuratibu mishahara ya wabunge.
Tume ya kitaifa ya mishahara iliratibu mishahara ya wabunge hao na kusema kuwa watapokea dola 6,300.
Wabunge hao, awali walisema kuwa wanapaswa kulipwa dola elfu kumi baada ya kusema kuwa wanafanya kazi kwa bidii.
Wabunge katika bunge lililopita walijilimbikizia dola 107,000 kama marupurupu ya kustaafu katika moja ya vikao vyao vya mwisho kabla ya uchaguzi mkuu mwezi Machi

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC