Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SUAREZ ASEMA KUIKATALIA REAL MADRID NI NGUMU

MSHAMBULIAJI Luis Suarez amezua hofu juu ya mustakabli wake katika klabu ya Liverpool baada ya kusema itamuwia vigumu kukataa ofa ya Real Madrid.
Suarez, anayetumikia kifungo cha adhabu ya mechi 10 kwa kumng'ata beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic, amesema katika mahojiano na kituo cha Redio cha Uruguay analazimika kuondoka kutokana na jinsi anavyoshambuliwa na vyombo vya habari England.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alisema: "Liverpool wanataka nibaki, lakini ngumu kuwakatalia Real Madrid.
Bombshell: Suarez has admitted he would be tempted by a move to Real Madrid
Mtikisiko: Suarez amesema itakuwa ngumu kuikatalia Real Madrid
"Nina familia ambayo pia inaathiriwa na hali hii na imevuka kiwango.
"Sijiandai kupambana na Waandishi wa Habari wa England. Nimepambana sana tangu nikiwa mdogo kufika hapa nilipo, kuwaacha waandishi fulani wanitendee ubaya. 
"Hawanihukumu kama mimi ni mchezaji, bali mtazamo wangu. Wananizungumzia kana kwamba wanafahamu maisha yangu yote vizuri. Nina mke na mtoto wa kike na siko tayari kuendelea kupambana na vyombo vya habari vya England,"alisema.
Liverpool imesistiza Suarez hauzwi na kwamba kwa kuwa alisani mkataba mpya wa miaka minne msimu uliopita, wanatarajia atabaki. 
International duty: Suarez is currently away with his Uruguay team-mates
International duty: Suarez is currently away with his Uruguay team-mates
Suarez kwa sasa yupo na timu yake ya taifa, Uruguay
International duty: Suarez is currently away with his Uruguay team-mates
Kocha Brendan Rodgers hana presha ya kumuuza mchezaji huyo, lakini Madrid wanaandaa Pauni Milioni 25 na wachezaji wawili, washambuliaji chipukizi Alvaro Morata na Jese Rodriguez.
Liverpool pia inakabiliwa na mtihani wa kumzuia kipa Pepe Reina anayetakiwa Barcelona ambaye amesema wazi itakuwa vigumu kukataa ofa ya vigogo wa Catalan.
"Ni vigumu kuwakatalia Barca, pamoja na kwamba sina uhakika kama wananihitaji kwa dhati,' alisema mlinda mlango huyo mwenye umri wa miaka 30.
Striking it rich: Aspas has been a revelation in his first La Liga season
Aspas amefanya vizuri katika msimu wake huu wa kwanza La Liga
Lakini Liverpool imeimarisha safu yake ya ushambuliaji kwa kukubali kumsajili kwa Pauni Milioni 6, mshambuliaji wa Celta Vigo, Iago Aspas, mwenye umri wa miaka 25, ambaye anaweza kucheza katikati au pembeni.
Huku Celta Vigo ikikabiliwa na hatari ya kushuka Daraja dau hilo ni punguzo kutoka Pauni Milioni 8 na Aspas atafanyiwa vipimo vya afya wiki ijayo.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC