Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Stars yapaa ikiahidi ushindi

KOCHA wa timu ya Taifa Stars, Kim Poulsen
Wakati timu ya taifa ya soka ya Tanzania (Taifa Stars) ilitarajiwa kuondoka nchini jana usiku kuelekea Addis Ababa kwa ajili ya kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Sudan, kocha wa timu hiyo, Kim Poulsen, amesema wanaichukulia mechi yao dhidi ya Morocco itakayofanyika Juni 8 mjini Marrakech kuwa ni zaidi ya fainali.

Stars itaanza kwa kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Sudan Jumapili Juni 2 katika kuwaandaa nyota wake kuzoea hali ya hewa ya baridi kama iliyoko Marrakech .

Akizungumza na gazeti hili jana asubuhi, Kim alisema kwamba wanafahamu ushindi wa aina yoyote ndiyo utakaowaweka kwenye nafasi ya kufuzu kucheza fainali zijazo za Kombe la Dunia.

Kim alisema kwamba wamejipanga vizuri kwa ajili ya mechi hiyo ya ugenini na kwamba ushindi wa 3-1 walioupata dhidi ya Morocco katika mechi yao ya awali hapa nyumbani unawaongezea kujiamini wakati wenyeji wao watakuwa katika 'presha' kubwa.

Mdenmark huyo alisema kwamba hakuna kisichowezekana katika mchezo wa soka na mwaka huu vijana wake wamedhamiria kuweka rekodi mpya kwa kufanya vizuri katika mechi hizo.

"Tunakwenda kuwafunga Morocco, hiyo ndiyo falsafa tunayoondoka nayo, tunafikiria fainali za Kombe la Dunia na CHAN (mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani) pia, tunaamini tutafuzu kwa sababu tunauwezo na tunapata ushirikiano wa kila aina kutoka kwa wanaotuzunguka," alisema Kim.

Nahodha wa timu hiyo, Juma Kaseja, alisema kwamba wamejiandaa vizuri na kila mmoja kwenye kikosi hicho ana kiu ya mafanikio.

Kaseja alisema kwamba wamedhamiria kutimiza ndoto za kushiriki fainali hizo kubwa zaidi duniani na vile vile kutangaza vyema jina la Tanzania.

"Inshaallah tutashinda, tunaamini hivyo na tumejiandaa vizuri, ni timu yenye chachu ya ushindi na mafanikio," aliongeza.

Timu hiyo inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro ilitarajiwa kuondoka jana saa 5:00 usiku kwa ndege ya Shirika la ndege la Misri ikiwa na wachezaji 21 ambao wanaongozwa na Kaseja.

Kikosi kilichoondoka kinawahusisha pia Mwadini Ally, Ally Mustafa, Shomari Kapombe, Kelvin Yondani, Aggrey Morris, Haroub Nadir 'Cannavaro', Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum Abubakar, Simon Msuva na John Bocco.

Wachezaji wengine ni Vicent Barnabas, Mudathiri Yahya, Athuman Idd na Haruni Chanongo huku nyota, Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu ambao wako na timu yao ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo watajiunga na kikosi jijini Marrakech, Juni 4 wakitokea Maputo, Msumbiji mara baada ya kuitumikia klabu yao katika mechi ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Liga Muculumana ya huko.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC