Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA, YANGA KUIPINGA AZAM

Klabu za Simba na Yanga zinafikiria kuupiga chini mkataba wa udhamini wa Kampuni ya SSB, ambao ni wamiliki wa timu ya Azam na badala yake kuukubali ule wa Super Sports.

Katibu Mkuu wa Yanga, Laurance Mwalusako alisema kuwa pamoja na kwamba hawajauona mkataba wa Super Sports, lakini uzoefu unaonyesha wanaingiza fedha nyingi zaidi kwenye ligi.
“Sisi tunasikia kuna mazungumzo yanafanywa na Kamati ya Ligi na TFF na Super Sports. Tunavyojua ligi za Uganda na Kenya, timu zinapata fedha nyingi. Mfano Uganda ni milioni 300 hawana shida ya mapato ya mlangoni, mechi ijaze, isijaze wao hawajali kwani tayari wana uwezo wa kujiendesha wenyewe kutokana na udhamini. “Sisi tulikataa wasionyeshe mechi bure, ila kama watakuja na ofa nzuri tupo tayari kupokea na kuachana na Azam kwani ofa yao ni nzuri zaidi.” alisema Mwalusako.
Hivi karibuni, TFF na Kamati ya Ligi walikutana na klabu za Ligi Kuu kujadili mkataba wa Azam, ambao wanatarajia kutoa Sh100 milioni kwa kila klabu msimu ujao kama udhamini ili kuonyesha mechi za ligi.
Hata hivyo kikao hicho kilizua mvutano mkubwa kwa klabu za Simba na Yanga kutaka kupewa udhamini mnono zaidi kwa vile ndiyo timu kubwa za soka na kudai hawawezi kupewa mgowo sawa na klabu nyingine.
Kuhusu vigogo hao wa soka kukutana na kupanga mikakati ya kupata mapato zaidi kwenye msimu ujao wa Ligi ikiwa ni pamoja na kuweka mkakati wa kuziachia mapato timu za mikoani Mwalusako alisema: “Hilo lipo juu ya uwezo wangu. Ni wenyeviti ndiyo walikaa na kuamua hilo.”

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC