Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SIMBA YACHUKUA WATATU LIBOLO




Mwenyekiti wa kamati ya usajili Hanspope

Na Pasko Linda

WACHEZAJI watatu wa klabu bingwa ya Angola, Recreativo de Libolo watajiunga na Simba SC kwa mkopo mwishoni mwa msimu, imeelezwa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe ameiambia mambouwanjani.blogspot.com 
jana kwamba, Libolo imekubali kuipatia klabu yake wachezaji hao watatu.
Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), hakuwa tayari kutaja majina ya wachezaji hao, lakini alisema ni beki wa kati mmoja, kiungo na mshambuliaji.
“Sisi tumezungumza na Libolo, wamesema watatupa kwa mkopo hao wachezaji, kwa kuwa hivi sasa tuna wachezaji watatu wa kigeni, tutaangalia namna gani tufanye ili tuwe na wachezaji wa tano kwa mujibu wa kanuni,”alisema Poppe.
Kwa sasa Simba SC ina Waganda wawili, Abbel Dhaira na Mussa Mudde na mshambuliaji Mzambia, Felix Sunzu. Beki Komabil Keita wa Mali amejitoa kwenye timu hiyo.
Simba SC ilitolewa na Libolo katika raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa kwa jumla ya mabao 5-0, ikifungwa 1-0 Dar es Salaam na 4-0 Angola.

Libolo imeonyesha ni timu nzuri kwa kufanikiwa kusonga mbele hadi kufika hatua ya makundi, baada ya mwishoni mwa wiki kuifunga Enugu Rangers na Nigeria mabao 3-1 Jumamosi.
Katika mchezo wa kwanza ugenini nchini Nigeria, Libolo ililazimisha sare ya bila kufungana.
Libolo wameingia katika uhusiano mzuri na Simba SC ambao unaonekana utainufaisha zaidi timu ya Tanzania, kwa kuanzia ni kupatiwa wachezaji hao watatu.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC