Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mwili wa Ngwair kuwasili kesho

Msanii wa bongofleva Albert Mangwea aliyefariki Jumanne nchini Afrika Kusini
Shirikisho la Muziki Tanzania kwa kushirikiana na Kamati ya Kuratibu Mazishi ya msanii wa bongofleva Albert Mangwea aliyefariki Jumanne nchini Afrika Kusini, limesema taratibu za kusafirisha mwili wa marehemu kuja nchini zinafanyika na mwili huo utawasili nchini kesho.


Mwili wa nyota huyo utaagwa Jumapili katika eneo bado halijaamuliwa kati ya viwanja Leaders, Biafra au Posta.

Msemaji wa kamati hiyo, Adam Juma, alisema baada ya mwili huo kuagwa, Jumapili jioni safari ya kwenda Kihonda, Morogoro itaanza kwa ajli ya mazishi yatakayofanyika Juni 3, mwaka huu.

"Tunaelewa namna Watanzania wanavyotambua mchango wa marehemu na jinsi alivyowahudumia kwa kuwaburudisha, hivyo tunawaomba wajitokeze kwa wingi siku hiyo katika kumuaga kijana wetu ambaye alikuwa nyota wetu sote," alisema Juma.

Juma alisema kwa kuwa gharama za kusafirisha mwili huo kutoka Afrika Kusini kuja Tanzania na kupelekwa Morogoro, vyakula, viti, matangazo na malazi ni kubwa hivyo wanaomba Watanzania wote kwa ujumla kutoa michango yao ya hali na mali ili kufanikisha msiba huo.

Akataja namba ya simu ya kaka wa marehemu Kenneth Mangwea 0754 967738 kuwa ndiyo itumike kwa michango hiyo.

Kwa upande wake, Addo November, ambaye ni Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania, aliwataka Watanzania kutoamini maneno yanayozushwa na watu na mitandao mbalimbali ya kijamii kuhusu sababu za kifo cha msanii huyo kwakuwa hadi jana hapakuwa na aliyekuwa akifahamu kilichomuua kwani uchunguzi wa daktari ulikuwa haujakamilika.

''Watu wanazusha maneno mengi kwamba eti kuna mtu kaununua msiba huu na ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini ndiyo unaosimamia taratibu zote za kusafirisha mwili wa marehemu.

Hayo yote si ya kweli kama utaratibu huo ungekuwapo sisi tungekuwa wa kwanza kujua lakini hakuna taarifa yoyote tuliyopata kuhusiana na mtu kuununua msiba huu, jambo lililopo ni kwamba wananchi wametoa michango yao kama kawaida,'' alisema November.

Meneja wa msanii huyo, Leo Rubama, ambaye amefanya nae kazi marehemu kwa muda wa miaka miwili iliyopita, alisema ameupokea msiba huo kwa masikitiko makubwa na hakuamini alipopokea taarifa hizo kwani aliona kama watu wanazusha.

"Nilishindwa kuamini kabisa nilipopokea taarifa hizo ukiangalia niliongea naye siku moja kabla ya mauti kumkukuta na akiniambia kuwa kesho yake niende uwanja wa ndege (wa kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam) kumpokea," alisema Rubama.

Mtayarishaji wa muziki katika studio ya Bongo Records, Paul Matthysen a.k.a P-Funk 'Majani', alisema msanii huyo alikuwa ni mtu mwenye upendo na ushirikiano mkubwa na alifanya kazi nyingi katika studio yake na kwamba itakuwa vigumu kwake kumsahau na kuamini kama hatamuona tena.

Shirikisho hilo pia liliwakumbusha Watanzania kumuombea msanii Mgaza Pembe a.k.a 'M to The P' ambaye alikuwa pamoja na Mangwair na amelazwa katika hospitali ya St. Hellen nchini Afrika Kusini.

Hali ya 'M to The P' iliendelea kutengemaa baada ya jana kuhamishwa kutoka katika wodi ya wagonjwa mahututi na kupelekea katika wodi ya wagonjwa wa kawaida.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...