Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LAMPARD AINUSURU ENGLAND KULALA NYUMBANI MBELE YA IRELAND

ENGLAND imetoka sare ya 1-1 na Jamhuri ya Ireland katika mchezo wa kirafiki usiku kwenye Uwanja wa Wembley.Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa William Collum wa Scotland, Ireland ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao ugenini, mfungaji Shane Long dakika ya 13, akiunganisha kwa kichwa krosi ya Seamus Coleman kutoka wingi ya kulia.

Frank Lampard aliwasawazishia wenyeji dakika 10 baadaye, yaani dakika ya 23 kuftaia kazi nzuri ya Daniel Sturridge ambaye aliambaa uipande wa kushoto wa box, kabla ya kummiminia krosi mfungaji, aliyemtungua kipa Glenn Whelan.
Ashley Cole alipewa kofia ya dhahabu baada ya kutimiza mechi 100 za timu ya taifa ya England leo. 
Katika mchezo huo, kikosi cha England kilikuwa: Hart/Foster dk46, Johnson/Jones dk46, Cahill, Jagielka, Cole/Baines dkl54, Walcott, Lampard, Carrick, Oxlade-Chamberlain/Milner dk87, Rooney na Sturridge/Defoe dk33.
Ireland: Forde, Coleman, O'Shea, St. Ledger, Kelly, Walters/Sammon dk82, McCarthy, Whelan/Hendrick dk74, McGeady/McClean dk68, Long na Keane/Cox dk66.
Level terms: Frank Lampard (right) pokes home the equaliser for England
Mwokozi; Frank Lampard aliifungia England bao la kusawazishaHeads I win: Shane Long nods Republic of Ireland ahead at Wembley against England

Furaha: Shane Long akishangilia bao lake
Tonderful: Roy Hodgson presents Ashley Cole with a golden cap to mark 100 appearances for England
Roy Hodgson akimkabidhi Ashley Cole kofia ya dhahabu kwa kutimiza mechi 100 England
On the slide: Ireland's Stephen Kelly makes a tackle on England's Theo Walcott
Stephen Kelly wa Ireland akimdhibiti Theo Walcott wa England
Off target: Wayne Rooney lobs a shot wide of the goal for England
Wayne Rooney akipiga shuti lililopaa
Getting shirty: England captain Ashley Cole sees his shirt pulled by Irleand's Seamus Coleman
Nahodha wa England, Ashley Cole akivutwa jezi na Seamus Coleman wa Ireland
Taking a tumble: Ireland's Shane Long and England's Gary Cahill battle for an aerial ball
Shane Long wa Ireland akipambana na Gary Cahill wa England
Level terms: Frank Lampard (right) pokes home the equaliser for England
Frank Lampard (kulia) akiisawazishia England

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

Ngao ya Jamii sasa ni Simba na Yanga

Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF limebadilisha kanuni za mashindano za Ngao ya Jamii kutoka timu nne na sasa utaratibu utakuwa kama zamani. Bingwa wa Ligi Kuu bara atacheza na mshindi wa kombe la CRDB Cup "CRDB Federation Cup, na endapo kama bingwa wa ligi na CRDB atakuwa ni mmoja basi mshindi wa pili kwenye Ligi Kuu ya NBC atacheza mchezo wa ufunguzi wa ligi yaani Ngao ya Jamii.  Hivyo ni rasmi ufunguzi wa wa ligi kuu mchezo  wa "Ngao ya Jamii msimu huu 2025-2026 ni Yanga na Simba watakutana.

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...