Ruka hadi kwenye maudhui makuu

KIIZA AITOSA YANGA, AIFUATA SIMBA KINESI

Hamis Kiiza
Wakati uongozi wa klabu ya Yanga umesema kwamba mshambuliaji wao wa kimataifa, Hamis Kiiza, amekalia kuti kavu kwa sababu klabu haina kiasi cha fedha ambacho amekitaja ili apewe mkataba mpya, Mganda huyo ameshikilia msimamo wake huo.


Kiiza ameutaka uongozi wa Yanga umpe Dola za Marekani 50,000 (Sh. milioni 80) kwa ajili ya kusaini mkataba mpya na pia umpe mshahara wa Dola za Marekani 3,000 (Sh. milioni 4.8) kila mwezi.

Kiongozi mmoja wa juu wa Yanga (jina tunalihifadhi) alisema kuwa endapo Kiiza ataendelea kuwa na msimamo huo, nafasi yake itachukuliwa kiulaini na kipa Mghana, Yaw Berko na kiungo Mnyarwanda, Kabange Twite.

"Licha ya mazungumzo na kumweleza msimamo wetu, alibaki na msimamo wake na hadi alipoamua kwenda kwao, alituandikia barua akieleza kwamba atakuwa tayari kusajili kwa Dola za Marekani 45,000 na si chini ya hapo,".

Kiongozi huyo aliongeza kuwa Kiiza anatakiwa akubali kushusha kiwango cha fedha cha usajili ili asajiliwe la sivyo nafasi yake itachukuliwa.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Abdallah Binkleb, aliliambia gazeti hili kuwa kamati yake bado iko katika mazungumzo na wachezaji hao watatu na itakapofikia mwisho itawasajili wawili.

Binkleb alisema kwamba kamati yake inafanya maamuzi ya kumsajili mchezaji baada ya kuridhishwa na kiwango cha mchezaji husika na kuridhiwa na vipengele vitakavyokuwapo ndani ya mkataba.

Alisema pia wanataka kumaliza zoezi la usajili wiki hii ili mapema wiki ijayo programu ya mazoezi ya timu yao ianze kwa ajili mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame).

Yanga ndiyo mabingwa watetezi wa mashindano hayo ambayo mwaka huu yatafanyika kuanzia Juni 18 hadi Julai 2 huko Sudan.

Kuna taharifa zinasemekana kuwa Kiiza anajiandaa kuwasili nchini lakini ataifuata klabu ya Simba ambayo imemunyeshea nia ya kumsajili, Kiiza alianza mazungumzo na viongozi wa Simba kabla mkataba wake haujamalizika 

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC