Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kibaden aanza kazi leo,achimba mkwara kwa Julio

Na Mwandishi Wetu

KOCHA mpya wa Simba Abdallah Kibaden Mputa (Pichani) ambaye amemaliza mkataba wake na timu ya Kagera Sugar  ameonyesha kumpiga mkwara mzito kocha msaidizi wa Simba Jamhuri Kihwelo 'Julio', Kibaden ambaye leo ameanza kazi ya kuinoa Simba katika uwanja wa Kinesi alitoa mkwara kwa Julio hivi karibuni
.

Akizungumza katika kipindi cha michezo kinachotangazwa na redio Magic Fm hivi karibuni , Kibaden aliyetua Simba kwa makataba wa miaka miwili na  kurithi mikoba ya Mfaransa Patrick Liewig ambaye amerejea nchini kwao kwa mapumziko ameonyesha kutomuogopa Julio na kudai ni sawa na mwanaye wa kumzaa.

Kibaden anasema kuwa Julio ni kijana wake na alikutana naye Simba mara mbili, Mara ya kwanza akiwa anaifundisha Simba ambapo Julio alikuwa mchezaji, Na mara ya pili alikutana naye kama msaidizi wake ambapo yeye alikuwa kocha mkuu na Julio msaidizi.

Hivyo Kibaden amesema kuwa yuko tayari kufanya kazi na Julio endapo Simba watamalizana naye kama kocha mkuu wa kikosi hicho kilichopokwa ubingwa wa ligi kuu ya bara na hasimu wake Yanga, Hata hivyo Kibaden amemalizana na Simba na sasa anainoa timu hiyo.

Kibaden alipigiwa chapuo kuchukua nafasi ya Liewig ambaye inasemekana anaweza kutoswa, Liewig ameiongoza Simba kumaliza ligi ikiwa katika nafasi ya tatu huku akitumia kikosi cha vijana yaani B.

Kwa kumchukua  Kibaden Simba itakuwa imeondokana na makocha wa kigeni kwani ilikumbwa na misukosuko mikubwa msimu huu hasa kudaiwa fedha na makocha wake wa kigeni ambao hulipwa mishahara mikubwa

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC