Ruka hadi kwenye maudhui makuu

JAYDEE AZIDI KUJIKAANGA MWENYEWE

Nyota wa muziki wa Bongofleva,Judith Wambura a.k.a Lady Jaydee
 
Nyota wa muziki wa Bongofleva,Judith Wambura a.k.a Lady Jaydee, amesema kwamba aliyoyaandika katika waraka alioutuma kwenye blogu yake kwamba viongozi wa Clouds Group "wanapita kila mahali kuhakikisha kila mrija unaomuingizia chochote unakatika", ni ya kweli na aliyaandika kwa nia njema.


Jaydee ameeleza hayo katika utetezi wake aliouwasilisha jana kwenye Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni kujibu tuhuma zinazomkabili katika kesi ya madai dhidi yake iliyofunguliwa na viongozi wa Clouds Mei 14, mwaka huu.

Katika hati ya madai, Clouds Group wanaiomba mahakama imuamuru msanii huyo awaombe radhi hadharani katika chombo kinachoheshimika kwa kuwachafua katika jamii, imzuie Jaydee na wadau wake kutoa kauli za kuwachafua walalamikaji, izuie taarifa zote alizotoa kwa kuzichapisha ama kurekodi ili zisiendelee kusikika/kufikiwa na yeyote, alipie gharama zote za kesi hiyo na pia alipie hasara ya jumla waliyopata walalamikaji kulingana na itakavyokadiriwa na mahakama.

Jaydee aliwasilisha hoja zake mahakamani hapo jana saa 2 asubuhi akiwa amefuatana na mume wake Gadner Habash na wakili wake, Gabliel Mnyele.

Hata hivyo, walalamikaji nao wameiomba mahakama kujibu hoja zilizowasilishwa na Jaydee na watawasalisha hoja zao mahakamani hapo Juni 3 mwaka huu. Kesi hiyo itasikilizwa kwa hakimu Athumani Nyamlani Juni 13, mwaka huu saa 5 asubuhi.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC