Ruka hadi kwenye maudhui makuu

BREAKING NEWS; BEKI HATARI LA THE CRANES LASAINI MIAKA MIWILI SIMBA SC


SIMBA SC imeendelea na harakati za ujenzi wa kikosi kipya hatari cha msimu ujao, baada ya saa mbili zilizopita kukamilisha usajil iwa beki wa kati wa kimataifa wa Uganda, Samuel Ssenkoomi anayechezea timu ya Mamlaka ya Mapato Uganda (URA).
Habari za  ndani ya Simba, zimesema kwamba Ssenkoomi amesaini mkataba wa miaka miwili kuchezea Wekundu hao wa Msimbazi.
Huyo anakuwa Mganda wa tatu katika kikosi cha Simba SC baada ya kipa, Abbel Dhaira na kiungo Mussa Mudde na inawezekana hadi wiki ijayo, Wekundu hao wa Msimbazi wakatimiza idadi ya wachezaji wanne kutoka nchi hiyo, kwani hivi sasa wako mbioni kuinasa saini ya mshambuliaji hatari mno wa The Cranes.  
Aidha, beki huyo mwenye nguvu na akili za mpira, anakuwa mchezaji wa tano mpya kusajiliwa Simba SC kwa ajili ya msimu ujao, baada ya awali kusajiliwa wachezaji wanne wazawa, kipa Andrew Ntalla kutoka Kagera Sugar, beki Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ kutoka Mtibwa Sugar, kiungo Twaha Shekuwe ‘Messi’ kutoka Coastal Union na mshambuliaji Zahor Pazi kutoka Azam FC aliyekuwa anacheza kwa mkopo JKT Ruvu.  
Simba SC imepania kuboresha kikosi chake ili kurejesha makali yake msimu ujao, baada ya  msimu huu kutoka mikono mitupu, ikivuliwa ubingwa na kukosa hata nafasi ya pili, ya kucheza Kombe la Shirikisho Afrika.  
Simba SC ambayo mzunguko wa kwanza ilikuwa chini ya Mserbia, Milovan Cirkovick na mzunguko wa pili chini ya Mfaransa Patrick Liewig, imemaliza Ligi Kuu katika nafasi ya tatu nyuma ya Azam na Yanga mabingwa.
Kocha Mfaransa Patrick Liewig amepewa mishahara yake ya miezi miwili, Sh. Milioni 12 aliyokuwa anadai na tiketi ya kurejea kwao moja kwa moja na Abdallah Athumani Seif, maarufu ‘Kingi Kibadeni’, bila shaka atasaini mkataba wakati wowote kurithi mikoba.
Liewig sasa atakuwa anadai mshahara wa mwezi mmoja, Mei ambao uko ukingoni yeye akiwa tayari Ufaransa.
Simba SC pia imewaongezea mikataba wachezaji wake chipukizi kadhaa iliyowapandisha kutoka kikosi cha pili akiwemo Haruna Chanongo, ambaye alikuwa anapigiwa hesabu na wapinzani wao wa jadi, Yanga SC.
Simba sasa inaelekeza nguvu zake katika usajili wa mshambuliaji sambamba na kusaini mikataba mipya na Nahodha wake Juma Kaseja pamoja na kiungo Amri Kiemba.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC