Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AKINA MBIYAVANGA WAONDOLEWA TENA NA KIBADEN SIMBA

Kocha mpya wa timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Abdallah 'King' Kibadeni
 
Wakati kocha mpya wa timu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Abdallah 'King' Kibadeni akiahidi kuanza kurejesha heshima ya kikosi hicho katika mashindano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame), tayari amewapiga 'panga' wachezaji wa kimataifa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambao walikuwa wakifanya majaribio.

Wachezaji hao ambao Kibadeni na wasaidizi wake hawajaridhishwa na viwango vyao ni Fabrice Baloko, Fabian Tshiyaz, Patrick Milambo na Joe Fills.

Akizungumza na mtandao huu Kibadeni ambaye aliiongoza Simba kufikia fainali ya Kombe la CAF mwaka 1993, alisema kuwa bado amewapa nafasi wachezaji wengine wawili, kiungo mkabaji kutoka Ivory Coast, Kouakou Martial na beki anayetoka Nigeria, Youssouf Gabra.

Aliongeza kuwa bado milango iko wazi katika kuangalia wachezaji wa kuwasajili na jana jioni zaidi ya nyota watatu kutoka klabu za Prisons, JKT Ruvu na JKT Oljoro, walitarajia kuanza mazoezi chini ya mshambuliaji huyo wa zamani wa Simba.

Kocha huyo alisema kwamba anataka kufanya usajili kwa umakini ili kuhakikisha msimu ujao Simba inafanya vizuri na anarejesha imani kwa mashabiki wake.

Kocha huyo mkongwe alisema kuwa kikosi hicho ambacho kiko katika mabadiliko kinahitaji muda ili kuweza 'kusimama' na kucheza kama timu hasa kufuatia uamuzi uliofanyika wa kujenga upya timu yenye mchanganyiko wa wachezaji chipukizi na wazoefu.

"Timu hii ina wachezaji wakubwa ambao wanatakiwa kuelimishwa na kubadilishwa kidogo na wachezaji vijana nao wanahitaji kuelimishwa ili kujua nini wanatakiwa kufanya kukabiliana na ushindani," alisema kocha huyo.

Aliongeza kwamba kikubwa anachokiangalia yeye ni wachezaji kuwa na nidhamu huku akisisitiza kutowarudisha wachezaji waliosimamishwa kwa kosa la utovu wa nidhamu.

Simba tayari imeshawasajili Issa Rashid kutoka Mtibwa, Zahor Pazi (Azam), Andrew Ntalla (Kagera Sugar), Ibrahim Twaha (Coastal Union) na Mganda Samuel Ssenkoomi wa URA ya Uganda.

Wakati huo huo, Simba inatarajia kucheza mechi ya kirafiki ya kimataifa Juni 12 mwaka huu dhidi ya Sofapaka inayoshiriki Ligi Kuu ya Soka ya Kenya.

Mratibu wa mchezo huo,George Wakuganda, alisema kuwa mchezo huo utatumiwa na Simba kutambulisha wachezaji wapya.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC