Ruka hadi kwenye maudhui makuu

AFYA NA JAMII



SABABU ZA MDOMO KUNUKA NA MENO KUOZA

Na Mwandishi Wetu

LIMEKUWA tatizo kubwa kwa binadamu wa aina zote wakubwa kwa watoto kusumbuliwa na maradhi ya meno ambapo sasa tatizo hili limezidi kupita kiwango.


Zamani ilikuwa imezoeleka watu wenye umri mkubwa hasa wazee walikuwa wakisumbuliwa na maradhi ya meno na kusababisha mdomo kutoa harufu kali inayotia kinyaa.

Lakini kwa miaka hii ya sasa matatizo ya meno kwa watoto na vijana wenye umri wa miaka 15-25 limezidi kuwa kero na kuwasababishia vijana hao kukosa raha kutokana na kuoza kwa meno yao na kutoa harufu mbaya.

Mkurugenzi wa kituo cha utafiti na tiba mbadala Dk Ndulumo amezungumzia maradhi ya meno na dalili zake huku akitoa tahadhali jamii kutopendelea kula vyakula fulani.

Dk Ndulumo ambaye ni mmiliki wa kituo chake cha tiba mbadala kijulikanacho Goligota Herbs, ameiambia MAMBO UWANJANI kuwa maradhi ya meno husababishwa na ulaji wa vitu vitamu pamoja na kutopendelea kusafisha meno kwa wakati.

Amesema kinywa cha binadamu kina bakteria wengi waliojificha ambao hushambulia mabaki ya chakula yanayosalia kwenye meno, Bakteria hao hula mabaki hayo na kuzishambulia fizi ambapo baadaye hukimbilia kwenye meno ya kuyala.

Meno huoza na kusababisha maumivu makali toka kwa kuathilika, Dk Ndulumo anasema, 'Kula vyakula vya moto sana, kutokupiga mswaki kikamilifu na kwa wakati hupelekea tatizo la kuoza kwa meno', alisema.

Aidha aliongeza kuwa kwa kawaida mswaki hutakiwa kutumiwa mara tatu kwa siku, Matumizi mabaya ya vyakula vyenye sukari nyingi mfani pipi na biskuti, alisema.

Alizitaja sababu nyingine zinazopelekea kuharibika kwa meno, 'Sabau za kimaumbile yaani kurithi, Matumizi kinyume ya meno mfano kufungulia kinywaji kama soda, maji na bia kwa kutumia meno', aliongeza.

'Kutafuna meno yenyewe nk, Tiba yake ipo, kwa upande wa tiba mbadala kuna dawa za uhakika ambazo mgonjwa huzitumia kwa kuweka kwenye mswaki kusukutua na kung'atia', alieleza.

Ili kuonana na Dk Ndulumo unaweza kumpigia simu kwa kutumia namba yake ya kiganjani 0713 690868 au fika katika kliniki yake iliyopo Kariakoo jijini Dar es Salaam

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC