Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MTANZANIA AZIDI KUTESA ULAYA

KIUNGO chipukizi Mtanzania, Adam Nditi jana aliendelea kuwa nje wakati timu yake, Chelsea ilipolala 1-0 mbele ya Norwich ugenini, bao pekee la Cameron McGeehan dakika ya mwisho kwa penalti katika Fainali ya kwanza ya Kombe la FA la Vijana.
Mechi ilionekana itaisha kwa sare hadi beki wa Chelsea, Alex Davey alipodaiwa na refa Neil Swarbrick kumuangusha kwenye eneo la hatari Joshua Murphy katika dakika ya pili ya dakika za nyongeza.
McGeehan hakuiangusha beji yake ya Unahodha na akaenda kuukiwamisha nyavuni mkwaju wa penalti akimtungua kipa Mitchell Beeney na kuwainia kwa shangwe mashabiki wa nyumbani, Uwanja wa Carrow Road ambao walikuwa zaidi ya 22,000. 
Chelsea ilitawala mchezo huo na kutengeneza nafasi nzuri, ambazo walishindwa kuzitumia, lakini waapewa nafasi kubwa ya kuupiku ushindi huo mwembamba katika mchezo wa marudiano nyumbani, Uwanja wa Stamford Bridge wiki ijayo.
Sasa ni mwezi wa pili, Nditi anayetokea visiwani Zanzibar anakosekana kabisa katika kikosi cha Chelsea, hata benchi hakai na haijulikani nini kinachomsibu kama ni majeruhi au amepokonywa namba.
Lakini BIN ZUBEIRY itaendelea kufuatilia ili kujua ukweli juu ya kiungo huyo aliyebeba matumaini ya Watanzania wengi kwamba ataling'arisha jina la nchi yake katika klabu kubwa Ulaya.
Kikosi cha Norwich City kilikuwa: Britt, Norman, Wyatt, McGeehan, McFadden, Toffolo, Murphy, Randall, Morris, King/Young na Murphy.
Chelsea: Beeney, Aina, Davey, Ake, Wright, Baker, Kiwomya, Loftus-Cheek, Feruz/Musonda, Colkett/Swift na Boga
Late: Norwich's Cameron McGeehan smashed home from the spot to give the Canaries a slender first-leg lead
La ushindi jioni: Nahodha wa Norwich, Cameron McGeehan akifunga kwa penalti. Chini anapongezwa na wenzake.
Norwich's Cameron McGeehan

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HISTORIA YA TIMU YA MASHUJAA YA KIGOMA, KUMBE NI SHEA YA JESHI NA WANANCHI

Timu inaitwa Mashujaa Lake Tanganyika FC ( Mashujaa FC ) ilianza rasmi kampeni yake ya kupanda Ligi Kuu tarehe 29/9/2018 na imepanda Ligi Kuu 25/06/2023 miaka mitano ya kupambana kwenye Ligi Daraja la kwanza Championship. Timu hii inaendeshwa kwa ushirikiano wa pande mbili kati ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji kwa niaba ya Wananchi wa Kigoma. Muelewe hapa maana wengi wanasema ni timu ya Jeshi asilimia 100% Nembo ya timu ni Sokwe Dume, Shujaa wa Hifadhi za Gombe na Mahale zilizopo mkoani Kigoma. Rangi ya kwanza ya jezi ya timu (first kit) ni hiyo hapo chini na kwenye nembo ya timu ni rangi za tunda la michikichi (mawese ). Hii kama njano ni mawese yaliyoganda na huo wekundu ni mawese ya moto. Ukishika tunda la Mse juu utaona wekundu na ukikata katikati utaona njano. Nyeupe ni ‘nazi’ ya Mse hizi ni alama za utajiri wa Kigoma Jezi nyingine ni blue inayowakilisha Ziwa Tanganyika na Jezi nyingine ni Nyeupe

MAKALA: SIMBA NI TIMU YA KWANZA TANZANIA KUINGIA NUSU FAINALI AFRIKA

Na Prince Hoza AFISA Habari wa klabu ya Yanga SC Ally Shabani Kamwe alidiriki kuudanganya umma wa wapenzi wa soka hapa nchini kwamba hakuna timu yoyote hapa Tanzania kuwahi kuingia hatua ya nusu fainali ya vilabu Afrika. Kamwe alisema timu yake ya Yanga itakuwa timu ya kwanza nchini kuingia nusu fainali ya Afrika, Yanga ilikuwa inakaribia kabisa kutinga nusu fainali ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ilianza vizuri ikiwa ugenini baada ya kuilaza mabao 2-0 timu ya Rivers United ya Nigeria, hivyo ilikuwa inasubiria mchezo wa marudiano uliofanyika uwanja wa kumbukumbu ya Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam. Kwa vyovyote Yanga walikuwa na uhakika wa kutinga nusu fainali kwani walihitaji sare yoyote ama ushindi wa aina yoyote. Hapo ndipo Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe aliamua kupiga vijembe kwa watani zake Simba SC na kuipotosha jamii kwa kudai kwamba Yanga itakuwa timu ya kwanza Tanzania kuingia nusu fainali ya Afrika. Kamwe ameifuta hadi rekodi ya Simba kuwa timu ya kwanza Tan...

Mabululu ni wa Simba SC

Simba wameweka donge nono kunasa saini ya mshambuliaji Agostinho Cristovan Paciencio Mabululu anayekipiga Al Tripoli ya Libya Ili ajiunge na Wekundu hao wa Msimhazi. Simba wamefanya mazungumzo ya moja kwa moja na wakala wa Mabululu na mchezaji mwenyewe na wako tayari kulipa kiasi cha juu zaidi kunasa saini ya mshambuliaji huyo hatari zaidi Simba wanahitaji kumalizana na mshambuliaji huyo badala ya kumaliza fainali ya kombe la Shirikisho, tayari Crecentius Magori yuko nyuma ya mpango huo kuhakikisha Simba ijayo inatisha. Mbali na Mabululu, Simba pia inahitaji Saini ya kiungo mshambuliaji wa Azam FC Feisal Salum "Feitoto" ambaye pia amewahi kuichezea Yanga SC