Na Salum Fikiri Jr, Shinyanga Stand United ya Shinyanga jioni ya leo imeibuka na ushindi mbele ya mashabiki wake dhidi ya Yanga SC katika uwanja wa CCM Kambarage kwa bao 1-0 mchezo wa Ligi kuu bara. Kama si bahati Yanga leo wangeweza kubugizwa mabao matatu kwani kikosi cha Stand kimecheza vizuri na kulitia msukomsuko lango la Yanga. Yanga imefungwa bao hilo katika kipindi cha pili baada ya kazi nzuri ya Kevin Sabato, Yanga ililala mbele ya 'Maproo' wake Donald Ngoma raia wa Zimbabwe na Amissi Tambwe wa Burundi huku pia ikiwa na mastaa wake wengine
Kwa habari na matangazo tunapatikana Kariakoo jijini Dar es Salaam au piga +255 652 626627 au +255 755 522 216 barua pepe princehoza@gmail.com