Benchikha aliwatahadharisha mapema Simba lakini hawakumsikia

Kocha wa zamani wa Simba SC, Abdelhak Benchikha amesema kwamba aliwaambia Simba wawe makini kwenye Idara ya ulinzi wanapocheza na Al Masry lakini hawakumsikia.

Hayo ameyadai baada ya kufungwa mabao 2-0 na kufifisha matumaini yao ya kutinga nusu fainali.

"Nilishawaambia hawa Simba kuweni makini sana kwenye safu yenu ya ulinzi maana hawa Al Masry wana washambuliaji hatari hawakunielewa mmeona
kilichotokea? Alilalamika Benchikha.