PICHA SABA ZA SHEREHE ZA UBINGWA YANGA SC

YANGA SC imefanikiwa kutetea ubingwa wake wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara hasa baada ya kufikisha pointi 72 ambazo hazitaweza kufikiwa na timu yoyote ile, kwa maana hiyo Yanga ni mabingwa msimu wa 2015/16.

Yanga ililazimishwa sare ya mabao 2-2 na Ndanda Fc ya Mtwara uwanja wa Taifa Dar es Salaam, zifuatazo ni picha saba kutoka uwanja wa Taifa Yanga wajisherehekea ubingwa wao waliokabidhiwa na waziri wa kilimo, mifugo na uvuvi Mhe Mwigulu Lameck Nchemba.

Nahodha wa Yanga Nadir Haroub 'Cannavaro' akinyanyua kikombe cha ubingwa wa ligi kuu msimu wa 2015/16
Wachezaji wa Yanga wakisherehekea ubingwa wao wa bara
Furaha ikiendelea uwanja wa Taifa wachezaji wa Yanga wakifurahia kikombe cha ubingwa wa ligi kuu bara
Mashabiki wa Yanga wakifyatua mafataki kufurahia ubingwa wa bara
Kocha wa Yanga Mholanzi Hans Van der Pluijm akiwa na baadhi ya wachezaji wa Yanga wakishikilia kombe lao
Kiungo wa Yanga Mzimbabwe Thabani Kamusoko akiwa amemshika mtoto wake  akifurahia ubingwa na familia yake wakifurahia ubinhwa
Mabingwa wa soka Tanzania bara Yanga Sc