Julio ataka viongozi Simba kujiuzuru kufungwa mara 5 mfululizo na Yanga

Kocha na mchezaji wa zamani wa Simba SC, Jamhuri Kihwelu 'Julio' anashangazwa na viongozi wa Simba kuendelea kukaa madarakani wakati wanafungwa mara 5 mfululizo na watani wao Yanga.

Julio kwa hasira anawataka baadhi ya viongozi wa Simba kuachia ngazi na kupisha wengine wenye uchungu na Simba huku akishauri kufungwa na Yanga ni kosa kubwa na si la kuzoeleka.

"Unafungwa na Yanga mara 5 Mfululizo alafu viongozi wapo tu, Simba sio mali ya mtu wakae pembeni waliokaa. 

Wana Simba wenye uchu na mafanikio timu waje waongoze,” Jamhuri Kihwelo amesema