Hatma ya Manula kubaki Simba ataamua Fadlu

Meneja wa habari na mawasiliano wa Simba Ahmed Ally amethibitisha kuwa mlinda lango Aish Manula ni miongoni mwa wa hezaji ambao mikataba yao iko ukingoni_

Hata hivyo amesema hatma ya mlinda lango huyo iko mikononi mwa benchi la ufundi kama watahitaji kuwa nae au la_

"Mkataba wa Manula unamalizika mwishoni mwa msimu lakini wenye jukumu la kuamua nani abaki nani aondoke ni benchi la ufundi"_

"Pamoja na kuwa Manula hakupata nafasi misimu huu lakini hilo halimuondolei sifa yake ya kuwa golikipa bora ambaye timu nyingi zingependa kuwa nawe"_

"Hatma yake itaamuliwa na benchi la ufundi na viongozi kile kitakachoamuliwa tutawajuza wanachama na mashabiki wetu," alisema Ahmed_

Kuna taarifa kuwa Manula yuko mbioni kurejea kwa waajiriwa wake wa zamani Azam Fc, ambapo anasubiri mkataba wake ufikie tamati mwishoni mwa mwezi huu_

Msimu huu umekuwa mgumu kwa Manula kwani hakupata nafasi ya kucheza mechi yoyote ya mashindano_

Shida ilianza baada ya mchezo dhidi ya Yanga msimu uliopita akikaa langoni na kuruhusu mabao matano katika mchezo ambao ulipelekea uongozi wa Simba umsimamishe kuchunguza tuhuma za hujuma.