Timu ya Mayele, Inonga uso kwa uso Ligi ya mabingwa Afrika leo

Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika (CAFCL) inaendelea kutimua vumbi leo Aprili 01, 2025 kwa michezo ya mkondo wa kwanza wa hatua ya robo fainali ambapo Mabingwa watetezi, Al Ahly ya Misri watatupa karata yao nyumbani dhidi ya Al Hilal ya Sudan.

Wababe wa Afrika Kusini, Mamelodi Sundowns watakuwa wenyeji wa Esperance ya Tunisia huku MC Alger wakiwa wenyeji wa Orlando Pirates.

Beki wa zamani wa Simba Sc, Henock Inonga Baka na mshambuliaji wa zamani wa Yanga Sc, Fiston Mayele watakutana uso kwa uso wakati Pyramids ya Mayele wakiikaribisha FAR Rabat ya Inonga.

16:00 Sundowns πŸ‡ΏπŸ‡¦ vs πŸ‡ΉπŸ‡³ Esperance
22:00 Ahly πŸ‡ͺπŸ‡¬ vs πŸ‡ΈπŸ‡© Al Hilal
22:00 Pyramids πŸ‡ͺπŸ‡¬ vs πŸ‡²πŸ‡¦ FAR Rabat
16:00 MC Alger πŸ‡©πŸ‡Ώ vs πŸ‡ΏπŸ‡¦ Pirates